aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Saturday, April 5, 2014

KUHUSU WACHIMBA KOKOTO WALIOFUKIWA NA KIFUSI DAR MCHANA WA APRIL 04.

6Inasemekana watu watatu waliotambuliwa kwa majina ya Msagala,Jacob na Mhando ambao ni  wakazi wa Bunju jijini Dar es Salaam wamefariki dunia mchana wa April 04  baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakichimba kokoto. 
Watu hao walikua wakichimba kokoto hizo kwenye machimbo ya Mtanzania mwenye asili ya Kiasia aliyefahamika kwa jina la Kara Arjan machimbo yaliyopo eneo la Bunju-Mbweni Dar es salaam.
Taarifa inasema kuwa machimbo hayo yalishapigwa marufuku kutokana na watendaji wake kufanya kazi katika mazingira hatarishi ambapo wachimbaji hao wakiwa kazini,sehemu ya machimbo hayo iliporomoka na kuwafukia.
Picha za kwenye tukio ambazo zinaonyesha pia juhudi za watu wakiendelea na uokoaji pamoja na miili ya watu waliopoteza maisha.
2
5
1
9

No comments:

Post a Comment