aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, March 19, 2014

WOLPER AACHANA NA MPENZI WAKE NA KUAPA KUTO KUOLEWA TENA NA MBONGO, SOMA HAPA

STAA wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper ameibuka na kudai kuwa, atafanya kila njia ili aolewe na mwanaume wa nje ya nchi na siyo Wabongo ambao hawathamini mastaa.clip_image001Akizungumza na Uwazi, Wolper alisema, amefikia uamuzi huo kwa sababu ana uchungu moyoni unaotokana na dhana waliyonayo wanaume wa Kitanzania juu yao, wakiamini kuwa ni wahuni tu hivyo kuwashusha thamani.
“Unajua Mtanzania anamchukulia staa kama chombo cha starehe tu na hawezi kumuoa kamwe na hata akimuoa basi hatamthamini kama wanavyothaminiwa wasanii wa huko nje.
clip_image001[7]“Kule bwana (hajataja nchi) mtu akimuoa staa, anampa kipaumbele. Anaweza hata kutumia fedha kuhakikisha anakuwa na staa na maisha ya mke wake yanakuwa yenye amani lakini hapa kwetu tunadharaulika sana ndiyo maana nimefikia uamuzi huu,” alisema Wolper na kuongeza:
“Unajua Watanzania wanaamini staa kuandikwa magazetini ni uhuni lakini wanasahau kuwa maisha yake na magazeti ni kitu cha kawaida kwa sababu ya kujulikana. Mimi sina haja ya kueleza sana lakini naapa kabisa, mimi siwezi kuolewa na Mbongo.”

No comments:

Post a Comment