aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, March 12, 2014

BONGO MUVI KUNA MASHOGA!


IMEBAINIKA kuwa ndani ya tasnia ya filamu Bongokuna baadhi ya wasanii wanaofanya mapenzi ya jinsia moja yaani mashoga, Risasi Mchanganyiko limenyetishwa.

Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Hilo limeibuka ikiwa ni siku chache baada ya Rais wa Uganda, Yoweri Museven, kupitisha sheria nchini mwake ya kupiga marufuku mavazi yasiyo na staha, uvunjifu wa maadili na mapenzi ya jinsia moja.
Uganda ipo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiunganishwa na nchi zaTanzania, Kenya, Rwanda, Burundi na Uganda yenyewe.


HABARI KAMILI
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vilivyomo ndani ya kundi hilo, baadhi ya wasanii wa kiume wanadaiwa kuwa ni mashoga, ingawa wanajifanya vidume vya mbegu.


“Wapo mashoga na mabwana zao tunawajua ila sema sasa kwa sababu huna ushahidi wa moja kwa moja na hujamfuma kwenye tukio, unashindwa kumtaja,” alisema msanii mmoja wa kike, Bongo.


“Yule…(analitaja jina la msanii mkubwa) bwana’ke alifariki na sasa ana mwingine lakini ndani ya Bongo Muvi anaonekana kiwembe kwa sababu ana msururu wa wanawake,” alisema.

AMSHAURI JK
“Ingekuwa vyema sana kama Rais Jakaya Mrisho Kikwete akafanya kama alivyofanya mwenzake wa Uganda, Yoweri Museven katika kupiga vita ushoga,” alipendekeza msanii huyo.


Msanii mwingine wa kike ambaye amekuwa kwenye tasnia hiyo tangu enzi za makundi ya sanaa kutamba runingani (jina kapuni) naye alikiri kuwepo kwa ishu hiyo lakini akadai wanafanya kwa siri sana.


“Kuna wasanii wanaonekana watanashati mbele ya jamii lakini ni chakula ya watu kwa kuwa wanapenda sana vitu vya bure,” alisema msanii huyo na kuongeza:

“Wapo wengi tu ndiyo maana katika maisha yangu sijawahi kutoka na mwanaume wa Bongo Muvi, ni wachafu sana. Siku zote wasanii wa kike ndiyo tunaoambiwa kuwa ni malaya, eti tuna tamaa na habari nyingi zinatuchafua siye lakini ukweli ni kwamba hata wanaume wana tamaa ya maisha mazuri na mwishowe wanageuzwa wanawake.”

HUYU YUPO TOFAUTI NA WENZAKE
“Sikia nikuambie, ni kweli hili suala lipo lakini si kwa wote na kuna baadhi huwa wanasingiziwa tu. Unajua nini? Unaweza kukuta mtu ana tabia tu ya kujipenda, lakini wengine wanasingizia kuwa eti ni mashoga – siyo kweli.


“Mfano hata uje na greda hapa, akitokea mtu anazungumza upuuzi eti JB, Dk. Cheni, Ray, Hemed PHD, Mlela au Dude ni mashoga, nitabishana nao mpaka mwisho. Hao ni watu ambao wanajipenda tu, sasa ukiwahusisha na huo ujinga nitashangaa sana. Sisemi kuwa wanatajwa ila sasa akitokea mjinga akaja na hoja hiyo, nitabishana naye,” alisema msanii mmoja ndani ya Bongo Muvi.

Msanii Hisani Muya ‘Tino’ aliwahi kuigiza kama shoga na kusababisha minong’ono kwenye jamii, katika filamu aliyoipa jina la Shoga lakini ilizuiwa na serikali.

Mwingine ni Dk. Cheni ambaye amecheza kama shoga kwenye filamu yake ya Nimekubali Kuolewa, ingawa bado haijatoka mpaka sasa.


Msanii huyo akizungumzia hayo, alisema: “Kucheza filamu kama shoga hakuna maana kuwa kweli ni shoga, ni kuvaa uhusika tu. Watu wasiwahusishe wasanii walioigiza kama mashoga kwenye hii skendo,” aliweka nukta msanii huyo mwenye maneno mengi.

WASIKIE WENYEWE
Baada ya kupata taarifa hizo, waandishi wetu waliwatafuta baadhi ya wasanii wa kiume Bongo wanaotesa na kuwauliza kuhusu ishu hiyo (wasanii hao hawamo kwenye orodha tuliyonayo).


Wa kwanza kuzungumza alikuwa ni Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni ambaye alisema: “Miye sina la kusema kuhusu hilo, ni vyema kama utamtafuta mwenyekiti (Bongo Movie Unity, Steve Nyerere) ndiye mwenye mamlaka ya kuzungumza masuala kama hayo.”



KULWA KIKUMBA ‘DUDE’
“Hilo suala la ushoga ndani ya Bongo Muvi lipo hata miye nalisikiasikia, lakini halina uthibitisho ila kusemwa linasemwa sana.”


STEVE NYERERE
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’: “Ni kweli taarifa hizo zipo, wasanii wakishakunywa pombe huwa wanafanya mambo ya ajabu sana kuashiria tabia zao halisi, mimi kama mwenyekiti wa Bongo Movie huwa ninaumia sana.


“Nitahakikisha nawafukuza mashoga wote hata kama tutabaki wawili katika kundi letu, bora wawe na heshima.”


MWAKIFWAMBA SASA
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba: “Hiyo ishu ni kweli ipo, ndani ya Bongo Muvi, mashoga wapo wengi sana, ila bado hatujapata ushahidi wa kuweza kuwataka hadharani.”

No comments:

Post a Comment