aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, March 12, 2014

REHEMA FABIAN ANANGWA KWA PICHA ZAKE CHAFU

MISS Kiswahili 2008 Bongo, Rehema Fabian amenagwa vibaya na wadau baada kutupia picha za utupu katika mtandao wa Instagram.

Rehema Fabian katika pozi.
Wakizungumza na paparazi wetu mara baada ya kuziona picha hizo ambazo zinamuonesha baadhi ya viungo vyake nyeti, mashabiki wa staa huyo walimponda wakidai wamemchoka kwa kupenda kupaisha jina lake kupitia picha hizo chafu.


“Anajidhalilisha sana, nahisi hajui thamani yake kwani mtu mwenye kujitambua hawezi kuweka picha zinazoonesha mwili wake ukiwa mtupu, asipo jirekebisha yatakuja kumkuta makubwa maana kila mmoja anaamini anajiuza,” alisema shabiki huyo aliyeomba hifadhi ya jina.
Rehema Fabian.
Shabiki mwingine aliyeona picha hizo mtandaoni, alichangia kwa kusema staa huyo hana lolote la maana analolifanya tangu atwae taji la u-miss zaidi ya kuweka picha za utupu kwenye mitandao ya kijamii.

“We kila siku habari zako ndiyo hizohizo, kwa nini usitafute kazi nyingine ya kufanya na kukuingizia kipato?” ilisomeka komenti hiyo katika mtandao wa Instagram.


Baada ya kupata malalamiko hayo ya kumponda Rehema kutoka kwa mashabiki tofauti, paparazi wetu alimcheki nyota huyo kupitia simu yake ya mkononi, alipopatikana alifunguka:
“Nimepiga mwenyewe na kuziweka katika ukurasa wangu, sasa nashangaa hao wanaosema eti najidhalilisha kwa lipi hasa?”

No comments:

Post a Comment