aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, May 30, 2014

SABABU 5 ZINAZOKUFANYA UOE AU KUOLEWA NA MTU AMBAE SI CHAGUO SAHIHI KATIKA MAISHA YAKO


KUNA baadhi ya sababu zinazosababisha watu kuoana pasipo kufanya 

maamuzi sahihi. Wanandoa wengi huingia katika ndoa wakitegemea mambo 
mengi kubadilika, kitu ambacho ni makosa yanayosababisha ndoa nyingi 
kuvunjika.Kabla ya kuoa/kuolewa unapaswaUjitambue Kwanzana ujiulize 
maswali kadhaa, kwanza jiulize;(1)Je huu ni wakati sahihi?(2)Kwa 
ninimtu huyu? na(3)Unamuoa au kuolewa na mtu atakaye kuwa sambamba na 
malengo yako katika maisha yako yote?Wakati kuna sababu kadhaa za 
kumuoa/kuolewa na mtu sahihi, pia upande mwingine kuna sababu kibao 
zinazopelekea watu kuoa watu wasio sahihi kwao. Kabla ya kusema 
"Ndiyo" zingatia sababu tano hapa chini zinazokufanya uoe au kuolewa 
na mtu ambaye si sahihiambae baadae hupelekea kutengana na kupeana 
taraka.(1) Tumekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu. Kuwa katika 
mahusiano kwa kipindi kirefu sio sababu pekee ya kufanikiwa kumpata 
mwenye mafanikio katika maisha yako, unaweza ukawa umemvumilia kwa 
muda mrefu na sasa ukaamua tu kwasababu umekwisha zoea tabia yake na 
kufuata usemi wa"maji ukisha yavulia nguo shartiuyaoge".(2)Msukumo wa 
Marafiki- Rafiki zangu wote wamekwisha OA/KUOLEWA....... itabidi na 
mimi nioe/niolewe. Kufuata mkumbo wa makundi katika jamii sii kitu 
kizuri, kwani ndoa siyokitu cha kubeep na kuacha. Jipange kwanza na 
muda ukifika basi itaingia katika ndoa yenye mpangilio mzuri wa 
maisha.(3) Sidhani kama nitaweza.Usipo jiamini na kujipenda mwenyewe 
sidhani kama itakuwa rahisi kumpenda mtu mwingine unayetegemea kuwa 
nae maishani.(4) Mategemeo ya kuboresha tabia ya mwenza wako. Tukisha 
oana nitambadilisha tabia. Cheti cha ndoa siyo leseni ya kumrazimisha 
mwenzi wako kubadilika kwa lazima. Jaribu kuwa na subira na kumtafuta 
mwenzi mnae endana nae kitabia.(5)PESA- Anakazi nzuri naamini ataleta 
pesa au anatoka katika familia ya kitajiri. Kunaukweli mkubwa katika 
misemo ya wahengayani "kama ukiowa kwaajili ya pesa, basi utazilipa" 
japokuwa kuwa na pesa sio vibaya, lakini hii haitazuia pia haizuii 
kuwa na muunganiko mbaya wa ndoa.Wanandoa wengi huingia katika dimbwi 
hili ambapo wengine hushinikizwa kuoa kulingana na taratibu za kimila 
au kidini. Lakini pia wazazi wakati mwingine huchangia ndoa nyingi 
kuvunjika, ikiwa ni kwa kuwachagulia wananandoa mke au mume.Vijana 
ambao bado hamjaoa au kuolewa"Jitambueni Kwanza", fikirini kwa kina 
kabla ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi ambayo yatawagharimu muda wenu 
na kupata mateso ya muda mrefu.

No comments:

Post a Comment