aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, May 30, 2014

MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KUPITA KIASI


Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini 
linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo 
huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono.Kuna watu ambao 
hawezi kulala bilakufanya mapenzi na huku wengine wakikosa uwezo wa 
kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu.Mtu anaweza kuwa na mke na 
kujikuta kila siku anatumia 'chakula cha usiku' kwa sababu tu hakuna 
wa kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa 
mahari.Hilo linaweza kuwa jambo jema kwaupande mwingine, lakini 
uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya watu wanaolalamika 
kupoteza hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la watu wapenda 
ngono.Pamoja na tatizo hilo, yapo madharamengine mengi ambayo mtu 
asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, 
hivyo ni vema tukajifunza ili tusiwe watu wa kuendekeza miili kiasi 
cha kulazimika kufanya mapenzi kila tunapokutana hata kwenye nguzo ya 
umeme na chini ya miti kwa vile tu miili imetaka kufurahika.Twende 
pamoja katika kutazama madhara hayo kwa kina.KUPOTEZA HAMU YA 
TENDO.Watu wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za 
kimapenzi kwa wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia 
zinazoweza kujitokeza wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa 
mara.Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea 
mwenzakiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu.Aidha 
kukinai haraka staili za kimapenzi kunatajwa kujitokeza kutokana na 
kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu 
moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza 
kumfanya mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza 
hamu naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa 
kikamilifu.KUUJAZA MWILI TAMAA KUBWA.Tabia ya kufanya mapenzi mara 
kwamara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini na kuufanya mwili uwe na 
msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo la ndoa bila kukosa na 
hivyo kumfanyamhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa 
chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi nakwa wakati gani?Watu 
wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao 
kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake.Hawa 
ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au 
kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa 
zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi.Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi 
mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo 
akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu 
ya penzi.KUPOTEZA RAHA KAMILI YA TENDO.Raha ya tendo hutegemea sana 
hisia iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, 
hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unawezakupoteza 
msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi 
kumaliza tamaa yako.Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu 
na msisimko wako utakuwa mdogo!KUPOTEZA NGUVU ZA MWILI.Madhara mengine 
yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na 
kupoteza nguvu nyingi za mwili.Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa 
wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke. 
Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za 
kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha.Sambamba na hilo mbegu za 
uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa 
dhaifu.KUPATA MAGONJWA.Kama tulivyojifunza kuwa watu wanaofanya 
mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa na hujikuta wanafanya mapenzi 
holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi, 
lakini ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa 
wanawake huwafanya waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri 
kutotoa ute unaoweza kuwakinga na michubuko wakati wakujamiiana na 
hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka 
ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.

No comments:

Post a Comment