aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Tuesday, May 27, 2014

PAPA ASHUTUMU MAPADRI WALAWITI KANISANI

Mkuu wa Kanisa Katoliki, Papa Francis. 
Mkuu wa Kanisa Katoliki, Papa Francis, amewasili Roma baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu Mashariki ya Kati ambapo alisema kuwa tabia ya baadhi ya mapadri Wakatoliki waliokuwa wakiwanyanyasa watoto wadogo kingono kanisani inaweza kulinganishwa tu na misa ya Mashetani.
Baba Mtakatifu alifanya ziara ambayo ilihudhuriwa na maelfu ya watu wa imani tofauti katika eneo hilo na wachambuzi wengi wamesema kuwa imekuwa ya kufana.
Wengi wanasema kuwa Baba Mtakatifu kulinganisha vitendo vibaya vya ngono walivyofanyiwa watoto na mapadri na misa ya mashetani ni lugha nzito hasa ikitambuliwa kuwa tayari Papa Francis amewahi kuomba msamaha kwa vitendo hivyo kote duniani.
Vitendo hivyo vimeharibia sifa Kanisa Katoliki kwa muda mrefu sasa.
Taarifa kutoka makao makuu ya Papa yanasema kuwa kwa mara ya kwanza tangu yeye achukue wadhifa wake anatarajiwa kukutana na wale walionyanyaswa na mapadri kingono.
Wakatoliki wengi walikasirishwa na vitendo hivyo na wamefurahi kuwa Papa anaweza kuomba msamaha na kisha akutane na walioathirika na wengi wanasubiri kusikia atakachowambia atakapokutana nao.
CHANZO BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment