aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, February 21, 2014

Msanii Bongo Muvi Anaswa Akijiuza usiku wa Manane….Steve Nyerere Amcharukia.

ILE skendo ya kukithiri kwa baadhi ya mastaa Bongo kujiuza imechukua sura mpya kufuatia msanii wa Bongo Movies, Isabella Francis ‘Vai wa Ukweli’ naye kunasa mtegoni, Ijumaa lina kisa kizima.
Tukio hilo la aibu kwa tasnia ya sinema nchini lilijiri usiku wa kuamkia Jumanne iliyopita, Sinza ya Vatican jijini Dar es Salaam ambapo baada ya kuumbuka, Vai alijikuta akiangua kilio na kuomba siri hiyo isisambae.
VAI WA UKWELI NI NANI?
Vai ni msanii wa filamu za Kibongo kwa muda mrefu. Amecheza filamu kadhaa zikiwemo Beautiful Liar (ya kwake mwenyewe), Family Apart, Good Fellow na nyinginezo.

Vai wa Ukweli akificha uso wake baada ya kunaswa.

MALALAMIKO KWA OFM
Ikiwa katika kutega ‘rada’ zake, Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers ilipokea malalamiko ya listi ya wasanii wa kike wa Bongo Muvi wakidaiwa kujishughulisha na uuzaji wa miili huku jina la Vai likiwa miongoni mwao.

MCHEZO WAANZA
Kilichofanyika, Vai aliwekewa mtego na kujikuta akiingia mzimamzima. Fuatilia uhondo wa mawasiliano kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno (SMS, tunazo):
OFM: Mambo Vai? Naitwa Salum, natokea Arusha ila kwa sasa nipo Dar, naomba kuonana na wewe.
Vai: Ili?

OFM: Kusema kweli nimetokea kukupenda, nimetafuta namba yako nikaipata nikaona nikutafute.
Vai: Muda sina.

OFM: Please usiniangushe, nitakupa chochote utakacho, nakuomba.
Vai: Nani kakupa namba yangu?

OFM: Sijakuelewa.
Vai: Umetumwa wewe, siyo bure.
OFM: Hivi mtu unaweza kutumwa kumpenda mtu jamani? Usinifanyie hivyo, nipe hiyo nafasi Vai, utafurahia.
ANAINGIA, ANATOKA
Vai: Oke, kwa nafasi umechelewa maana boy ninaye. Kwani umefikia wapi?
OFM: (OFM yamdanganya) niko hoteli moja inaitwa Lunch Time hapa Tip Top Manzese (Dar), wewe uko wapi?

Vai: Mwananyamala (Dar), njoo nikuone.
OFM: Nimekuja huku Kariakoo kufungasha mzigo, we huwezi kuja pale hotelini baadaye? We si ni mwenyeji sana Dar?
Vai: Siwezi.
OFM: Sa tunafanyaje wangu? Nitaumia sana kama nitaondoka bila kukuona, nakupenda.

Vai: Ndo hivyo ukiweza njoo Mwananyamala.
OFM: Huko mimi ni mgeni wangu, nitalipia gharama zako, usininyong’onyeshe.
Vai: Tuma hela ya Bajaj kwa …(unatajwa mtandao) nitakuja.
OFM: Sawa nitakutumia, ni shilingi ngapi kutoka huko hadi hapa hotelini?
Vai: Kumi na tano tuma.

OFM: Sawa na ofa yako tukionana ni shilingi ngapi?
Vai: Ofa ya nini?
OFM: Si tukionana jamani ili nijiandae nisije nikaumbuka, unajua tena watu kama nyie…
Vai: We sikuelewi kwani kuna nini tofauti, kuonana umetaka nimekubali bado unaongea tofauti.
OFM: Tofauti vipi jamani?
Vai: Unazingua.

OFM: Nazingua vipi?
Vai: Tuma hiyo hela nije.
OFM: Pesa ya kujia siyo ishu, natuma twenty (20,000), nataka kujua shilingi ngapi utataka kuwa na mimi kwa leo ili nijiandae wangu, naomba uelewe.
Vai: Tutaongea usijali.

OFM: Kwa hiyo wangu, niambie basi.
Vai: Usijali nikija tutaongea.
OFM: Nataka ukija nisisumbuke, we niambie tu unataka shilingi ngapi kwa kuwa na wewe leo, nataka nikachukue pesa ATM, we mtu mzima bwana!

Vai: Oke siwezi, achana na mie. By the way mimi sijiuzi.
OFM: Siyo suala la kujiuza Vai, kama unataka nikukose sawa lakini ningefurahi sana, kuwa nawe, acha pesa, nitakupa utakachotaka.
Vai: Siwezi.
OFM: Usinifanyie hivyo utaniumiza.

Vai: Si nimekuambia tuma nauli nije? Tutaongea hujiamini.
OFM: Ujue nakuuliza hivyo ili nijipange hata kama ni kuchukua pesa nichukue za kutosha kwa leo.
Vai: Kama huelewi basi.
OFM: Kama sielewi nini? We niambe tu.
Vai: Milioni.

OFM: Milioni moja?
Vai: Ndiyo.
OFM: Usikomae Vai, nimetumia pesa nyingi kufungashia mzigo, nifanyie fea wangu. Hiyo m moja tutalala?
Vai: Siwezi.
OFM: Huwezi kulala? Sikia, nifanyie laki tano basi, ila itakuwa poa kama tutalala maana mshikaji niliyekuja naye kaondoka leo.

Vai: Kulala siwezi.
OFM: Kwa mfano kuanzia saa moja mpaka saa ngapi hivi naweza kuwa na wewe? Labda nikuambie ukweli, kwa nini nimekutafuta, kuna picha yako niliichukua kwenye gazeti  nikakupenda sana, nikawa namaliza shida zangu, nimekuja Dar ndo nikasema nikutafute unipe live kwa gharama yoyote Vai.
Vai: Kimya.

OFM: Subiri kidogo wangu nakutumia.
Vai: Mh! Kwa nini muda unaenda, kama umebanwa basi siku nyingine.
OFM: Noo please kuna mtu nimemwambia akutumie 15 (15,000/=) sasa hivi wangu, mambo mengine ukija, ukiipata niambie, sawa ee..
Vai: Mh!
OFM: Nini jamani tena?

BAADA YA DAKIKA NANE
Vai: Oke nimekuelewa. Nimeipata
OFM: So unatoka huko saa ngapi? Kwani ni mbali?
Vai: Ndiyo, wewe uko wapi?
Vai: Nikija sitaki uswahili, mie naogopa magazeti, sawa kaka, sasa unanipa changu nafanya kazi yako.
Vai: Nipigie.
Vai: Uko kwa wapi maana mimi nipo Vatican (Sinza, Dar).

KABANG!
Baada ya kuchati kwa muda mrefu bila kujua anaingia mtegoni, hatimaye Vai alifika kwenye Kituo cha Daladala Vatican lakini hakutaka kushuka kwenye Bajaj.
Badala yake alimtaka kachero wetu ambaye ni Salum wa bandia kuingia kwenye usafiri huo kisha akamuongoza dereva kuelekea Baa ya Mawela iliyopo jirani na eneo hilo.
Akiwa amejiaminisha kuwa analamba laki tano yake, Vai alianza kuagiza pombe za bei mbaya huku akisisitiza kupewa chake kwanza ili akampe huduma.
HALI YABADILIKA GHAFLA
Hata hivyo, hali ilibadilika ghafla, hebu fuatilia mazungumzo yao:
Vai: Vipi mbona kama hujiamini? Kabidhi laki tano yangu kieleweke.
Kachero wa OFM: Vai sikiliza, mimi si pedeshee wala mfanyabiashara wa Arusha. Ni kachero wa OFM (Oparesheni Fichua Maovu) ya Global Publishers. Tunafichua uovu ndani ya jamii.
Vai: (huku akihamaki) kaka hebu nioneshe ‘toileti’ zipo wapi hapa?

Kachero wa OFM: Toileti zile pale.
Vai alikwenda toileti ambako alikaa huko takriban dakika tatu. Cha ajabu, alirejea akiwa analia ambapo mambo yalikuwa hivi:
Vai: Unasema wewe ni mwandishi wa Global? Si kweli, nawajua wote ila wewe siyo!
Kachero wa OFM: Unatakiwa kusadiki haya niyasemayo.

Vai: Kama kweli nioneshe kitambulisho.
Kachero wa OFM: (huku akikitoa) hiki hapa.
Vai: Hamna. Kama ni kweli niitie Sifael (Paul) na Erick (Evarist) waje hapa.
Kachero wa OFM: Hakuna shida Vai, twende ofisini Bamaga-Mwenge wamejaa tele usiku huu.

Baada ya kusikia hivyo, Vai alinyanyuka na kwenda eneo la kuegesha magari na kuzua tafrani, ndipo kijana mwingine wa OFM aliyekuwa akilinda usalama wa mwenzake akatoa vifaa vyake vya kunasia matukio ambapo alimrekodi Vai akizua timbwili bila kujua.

Mbele kidogo ya baa hiyo, Vai aliita Bajaj na kumwagiza dereva amkimbize Global Publishers.
Alifika kwenye ofisi za gazeti hili akiwa anahema mithili ya mbogo aliyejeruhiwa ambapo alitulizwa na wahariri waliokuwa mzigoni na kufanya mahojiano:

USO KWA USO NA WAHARIRI
Wahariri: (wakijifanya hawaelewi chochote) nini kimetokea Vai?
Vai: Ninyi mnajua kila kitu. Kwa nini mmeniwekea mtego? Kuna jamaa anadai ni mwandishi wenu, alijifanya mfanyabiashara akawa anawasiliana na mimi.
Wahariri: Mlikuwa mnawasiliana kuhusu nini?
Vai: Alisema sijui aliniona kwenye gazeti akanipenda, amekuja Dar akaamua kunitafuta.
Wahariri: Kukutafuta kwa nini?

Vai: Alitaka akalale na mimi kwa laki tano.
Vai: Tulikubaliana tukutane lakini mimi sikuwa na mpango wa kwenda kulala naye. Nilitaka nichukue hiyo laki tano yake nimpe sababu za ‘kiwanawake’ so nisingefanya naye ngono.

Wahariri: Ina maana huwa unafanya hivyo? Huoni hatari kuchukua fedha ya mtu na kuingia mitini? Huo si ni utapeli? Huogopi kutafutwa na kufanyiwa kitu mbaya?
Vai: Naamini angenielewa tu (kilio mfululizo).

STEVE NYERERE, MTITU
Baada ya Vai kukiri kuingia kwenye mtego wa kujiuza, gazeti hili liliwasiliana na baadhi ya viongozi wao kuwasikia wanalizungumziaje tukio hilo.
Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity alisema: “Tunawafukuza wote mnaowanasa, hawana sifa ya usanii, wanaingia kutimiza ndoto zao za kujiuza. Hawafai Bongo Muvi.”

Naye Katibu wa Bongo Movie Unity, Wiliam Mtitu alifunguka: “Tutakaa kikao tumfukuze Bongo Muvi, ametuchafua sana.”
Mmoja wa mastaa ambaye hakutaka kutajwa jina alidai kuwa umefika wakati kwa mastaa kujilinda wakitajwa warembo kama Wema Sepetu, Jokate Mwegelo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Aunt Ezekiel, Jacqueline Wolper na wengine kwamba siku wakinaswa itakuwa ni aibu kubwa.

WENGINE KWENYE ‘TAGETI’
Listi ya mastaa wanaojiuza kwa mapedeshee iliyopo mikononi mwa OFM ni ndefu, kikosi bado kiko mzigoni kuwanasa.

KAZI NZURI YA OFM
Tangu OFM imeanza kazi yake nzuri ya kufichua maovu, kabla ya Vai tayari ilishawanasa mastaa watatu wa Bongo Muvi, Jacqueline Pentzel ‘Jack wa Chuz’, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ na Baby Joseph Madaha.

No comments:

Post a Comment