aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Sunday, February 23, 2014

MADHARA YA PEMPAZI AU PEDI....SOMA HAPA UKIACHA SHAURI YAKO !!


 
 
Kumekuwa na ongezeko kubwa la magonjwa ya mfumo wa mkojo (UTI) na uzazi kwa wanawake, hii inasababishwa na sababu nyingi ikiwemo ya kukosa uelewa sahihi wa kanuni za afya na usafi wa mwili pamoja na mazingira yanayomzunguka mwanamke. 
 
Mada za usafi wa mwanamke ni pana sana siwezi kumaliza kusema kila kitu, hivyo leo nitajikita zaidi katika matumizi sahihi ya pedi na mambo ya kuzingatia kabla ya kunua pedi. Wadada wengi wamekuwa wakitumia pedi na kuziacha zikizagaa mitaani hali inayofanya nijiulize kama tu ameshindwa kujua sehemu sahihi ya kuhifahi au kutupa pedi aliyotumia yeye mwenyewe, 
Je anauelewa upi katika matumizi sahihi ya pedi hizo kabla hajazitumia?
 Somo la leo nitajikita katika njia sahihi ya kuchagua na kutumia pedi, makosa yanayofanywa katika matumizi ya pedi na ushauri juu ya matumizi sahihi ya pedi na vitambaa kwa wale wanaovitumia.

Yafuatayo ni makosa yanayofanywa katika uchaguzi na matumizi ya pedi kwa wanawake:

1. Kutonawa mikono kabla na baada ya kutumia pedi. Mikono hushika sehemu mbalimbali hivyo kuna uwezekano ikawa na vimelea vinavyosababisha magonjwa kwa hiyo kushika pedi bila kunawa mikono kwa sabuni kunaweza kuhamisha vimelea hivyo kutoka mikononi na kwenda kwenye pedi inayotegemewa kuvaliwa.

2. Kutunza pedi bafuni au chuoni. Wadada wengi hupendelea kutunza pedi zao chooni/bafuni. Vyumba vingi vya choo/bafu havina mwanga wa kutosha na kuwa na unyevunyevu hali inayoweka mazingira mazuri ya ukuaji wa vimelea vya magonjwa kama bacteria na kitendo cha kutunza pedi katika sehemu hizo kunaweza kusababisha kuhama kwa vimelea hao kutoka bafuni/chuoni kwenda kwenye pedi isiyovaliwa na kupelekea pedi hizo kuwa na vimelea vya magonjwa na mwanamke anakuwa katika hatari za kupata maambukizi.

3. Kutoangalia muda wa matumizi wa pedi kabla ya kutumia au baada ya kuzihifadhi kwa muda mrefu hali inayopunguza kiwango cha ufanisi cha pedi sababu ya kuisha kwa muda wake wa matumizi.

4. Kununua pedi zinazouzwa kiholela kwa njia ya utangazaji na za bei rahisi (promotion) ambazo baadhi zimeonekana kutengenezwa kwa malighafi zilizo chini ya kiwango au kukaa kwa muda mrefu hivyo kuuzwa kwa bei rahisi ili zitoke na kutumika haraka kabla ya kuisha muda wake.

5. Kutumia pedi ambazo zipo katika majaribio maalum. Kama tunavyojua kuna kila aina za pedi mpya katika soko kwa kadri siku zinavyozidi kwenda na baadhi ya pedi huingizwa sokoni kinyemela pasipo tafiti za kutosha na bila hata kuthibishwa na mamlaka husika.

6. Kutumia pedi kwa muda mrefu. Wanawake wengi hususani katika nchi zinazoendelea huwa hawamudu kutumia pedi moja kwa muda wa masaa mawili kama inavyoshauriwa na wataalamu hivyo kujikuta katika hatari ya kupata magonjwa ya mfumo wa mkujo na njia za uzazi .

7. Kupendelea pedi zenye uwezo mkubwa wa kufyonza unyevunyevu ili ivaliwe muda mrefu pia ni tatizo sababu kwa kadri muda wa kuvaa pedi moja unapozidi kuongezeka na hatari za maambukizi ya magonjwa pia inazidi kuongozeka.

Wanawake wanashauriwa kufanya yafuatayo ili kuhakikisha usalama wa afya zao :

1. Kunawa mikono vizuri kwa sabuni kabla ya kugusa pedi ambayo unatarajia kuivaa na baada ya kuvaa kunawa tena mikono vizuri.

2. Kutohifadhi pedi bafuni au chuoni au sehemu yote yenye unyevunyevu na isiyo na mwanga wa kutosha ili kutotengeneza mazingira ya kukua kwa vimelea vya magonjwa ndani ya pedi.

3. Kuangalia kwa makini muda wa matumizi ya pedi kabla ya kununua au baada ya kutunza pedi kwa muda muda mrefu ili kuepuka kutumia pedi zilizopita muda wake wa matumizi.

4. Kuepuka kununua pedi zinazouzwa kiholela na zisizothibitishwa na TBS na mamlaka nyingine zenye dhamana ya kuangalia ubora wa pedi hizo. Mwanamke anatakiwa kuangalia nembo ya uthibitisho wa mamlaka hizo na kujiridhisha kuhusiana na usalama wa pedi hizo kabla hajanunua.

5. Kubadilisha pedi kila baada ya masaa mawili, kama tunavyojua damu ni moja wapo ya chakula kizuri sana kwa vimelea vya magonjwa kama bacteria ,unyevunyevu unaosababishwa na kuvaa pedi kwa muda mrefu pia unapelekea ustawi wa bacteria hao na joto ambalo lipo katika maumbile ya ndani ya mwanamke vikiungana kwa pamoja vinatengeneza mazingira mazuri ya ukuaji wa bacteria , hivyo wanawake wanashauriwa kutovaa pedi hizo kwa muda usiozidi masaa mawili ili kuepuka mazingira hayo.

6. Kuchagua aina sahihi inayokutosha ina kuepuka pedi zinazobana sana kupita kiwango sababu zinaweza pia kukufanya usiwe huru na kutengeneza joto la ziada na michubuko katika maumbile ya mwanamke,hivyo mwanadada unashauriwa kutumia pedi itakayokukaa vizuri(isilegee sana wala kuachia sana)

7. Kwa wadada wanaotumia vitambaa badala ya pedi ni muhimu pia kuzingatia kanuni za kiafya na usafi kabla na baada ya kutumia vitambaa hivyo kama vile kuchagua kitambaa angavu ,kukiloweka na kukifua vizuri, kuanika kwenye sehemu yenye mwanga wa jua wa kutosha na upepo wa kutosha pasipo na unyevunyevu ,kupiga pasi kabla ujakihifadhi na kabla ya kutumia ili kuuwa vimelea vya magonjwa na kuvitunza sehemu nzuri ambayo haina unyevunyevu, penye hewa na mwanga wa kutosha na mwisho ni kubadilisha kitambaa hicho kila baada ya masaa mawili pamoja na kunawa mikono vizuri kabla na baada ya matumizi ya vitambaa hivyo.

No comments:

Post a Comment