aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, February 5, 2014

HAYA NDIO MAISHA YA WEMA NA DIAMOND KABLA YA KUWA MASTAA...!KWELI TUMETOKA MBALI..


Ukitaka kujua kuwa ku-shine hapaBongo ni juhudi zako tu mwenyewe za kupiga kazi usiku na mchana,bila kulala na mwisho wa siku kufikia malengo yako,its true kwamba yapo majanga ya hapa na pale yanayoweza kumkatisha mtu tamaa yakufika malengo  ila Hapa town kila kitu ni possible tu,hata kama mtu una ndoto za ku-push Benz. Celebs hawa hawakuanza moja kwa moja tu kama mtu unavyodhani kuwa walipitia njia rahisi hadi kufika walipo.


diamond_3
Kuna Jamaa mmoja alikua akipanda basi na Naseeb Abdul (Diamond)  mwaka 2005 katika  kituo cha Shule Tandale Magharibi kipindi hicho hakufikiria kama jamaa angefika alipo sasa.
Mwaka 2008 na 2009 alikuwa akifanya kazi katika kiwanda cha mabegi kilichoko Mikocheni na kulipwa mashahara wa shilingi 2,000 kwa masaa 8, huku nauli ikimgharimu shilingi 1,000 mpaka kufika kwao na hapo chakula ni zaidi ya shilingi 1,000. “Ukimuona mtu ana mafanikio kiukweli ujue amehangaika sana, mimi katika maisha yangu sikuwahi kufikiria kama ningelikuja kupanda ndege kwa kutumia pesa yangu, namshukuru sana Mungu na haya ni matunda ya kazi ngumu ambazo huwa nazifanya,”  , haya ni maneno ya diamond aliyowahi kuyasema katika tamasha la fursa. Diamond hivi sasa ndio msanii pekee wa bongo anayeingiza mkwanja mrefu zaidi hapa town,na hiyo si tu mauzo ya kazi zake,ila pia show zake azifanyazo , mikataba ya kibiashara na biashara zake mwenyewe anazozifanya. 

Wema-Sepetu
Huku nyuma nae Wema Sepetu,kabla hata hajachukuwa taji la missTanzania,alikuwa mtu wa kawaida tu,taji ambalo ndio kwanza lilimtambulisha Celeb huyu hapa town,hata kama kuna mtu alishawahi kukutana na wema enzi hizo kwenye daladala sidhani kama atakuwa anamkumbuka.ila kama ni umiss tu ndio unadhani ulimpa shavu Wema hadi kufikia level hii alipo hivi sasa utakuwa umekosea,cause kuna mamiss wengi ambao hivi sasa hakuna hata mtu anayekumbuka kama alishawahi kuwa miss,ila kwa Diva huyu aliweza ku-rise na kufanya kazi kwa bidii ku-keep status yake,kipaji chake kizuri cha kuigiza ndicho kiliongeza popularity ya jina la Wema sepetu hapa town na kwa kila movie ambazo amecheza msanii huyu,zina historia ya kufanya mauzo ya hali ya juu,hivyo kuzidi kuonyesha kazi yake nzuri na watu jinsi wanavyoikubali. 
Wema-Sepetu-Diamond-Platnumz-Sasa-copyright-www-vibe-co-tz 

Mambo yalikuwa kama hivyo,angalia transformation ya hao celebz enzi hizo za mwalimu na hivi sasa kama uliweza kutafakari wangeweza kufika hapa na ku-shine kama wanavyo-shine hivi sasa,hapa town hakuna mtu aliye-rise tu na kushine moja kwa moja,kila mtu alianzia somewhere,enzi hizo haikuwa na story za sembe kama ilivyozagaa hivi sasa,sinadhani hata wenyewe hawakuweza ku-imagine kama wangeweza kuwa popular kama hivi sasa,bali ni hustle zao ndio ziliweza kuwaweka hapa town,hadi hivi sasa kufikia kuwa moja ya celebs  wanaongoza kuongelewa zaidi katika siku au hata kwa mwaka kuliko celeb yeyote hivi sasa hapa Bongo…

No comments:

Post a Comment