AMA kweli dunia imefika ukingoni! Ile Oparesheni Fichua Maovu (OFM) , bado ipo kazini ikishirikiana na polisi ambapo safari hii imeibuka na kigongo cha aina yake baada ya kumnasa ‘mwanaume tata’ akijihusisha na ukahaba....
Mwanaume tata baada ya kunaswa na OFM akijihusisha na ukahaba.
Mbali na jamaa huyo ambaye jina lake halikupatikana, baadaye ilibainika kuwa kulikuwa na wenzake wawili ambao ilikuwa vigumu kuwatambua kufuatia kujiremba kupita hata wanawake wenyewe.
...Akiwa mikononi mwa polisi akipelekwa kwenye difenda.
Mara baada ya kunaswa, kijana huyo aliangua kilio huku akidai kuumbuka kwani familia yake wakiiona picha yake hawatamwelewa.
“Naombeni tumalizane hapahapa kwani nyumbani hawafahamu kuwa nipo hapa muda huu. Hii ni kesi kubwa kwangu nisaidieni,” alisikika kijana huyo.
...Akiwa ndani ya difenda na wenzake walionaswa katika tukio hilo la kufanya ukahaba.
Wakazi wa maeneo hayo walikuwa wakilalamika mara kwa mara kutokana na kurundikana kwa makahaba mahali hapo na kusababisha uchafuzi wa mazingira kwa kutupa ovyo mipira ya kiume (kondom).
Katika msako huo, wanaume hao watatu walijumuishwa na wanawake 20 waliokamatwa wakijihusisha na biashara haramu ya kuuza miili.
No comments:
Post a Comment