aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 31, 2013

MWALIMU AFUMWA CHINI YA KITANDA CHA MWANAFUNZI WAKE WA KIKE...!!



Mwalimu wa somo la Hisabati amebambwa akiwa amejificha chini ya kitanda cha mmoja wa wanafunzi wake mwenye umri wa miaka 16.
Mwalimu huyo ambaye hakutajwa jina, mwenye miaka 35, aligundulika pale mama wa binti huyo aliporejea nyumbani kumtazama binti yake katika siku ya mwisho ya muhula.

Alikamatwa na Polisi wa Greater Manchester kwa tuhuma za kutumia vibaya nafasi yake ya uaminifu kisha akaachiwa kwa dhamana lakini amesimamishwa kazi.

Mama huyo aliwabamba wawili hao katika chumba cha binti yake baada ya kurejea kwenye nyumba ya familia iliyoko Bolton, Manchester, katika siku ya mwisho ya binti huyo ya muhula.

Chanzo kimoja kilieleza: "Wawili hao walirejea nyumbani kwa binti huyo sababu walijua hakuna yeyote angeweza kuwapo pale.

"Lakini mama huyo alikuja nyumbani mapema kuliko ilivyodhaniwa na kuwabamba.

"Alikwenda chumbani kwa binti yake na kukuta mwalimu huyo akiwa amejificha chini ya kitanda. Ulikuwa mshituko mkubwa. Mama huyo alipagawa."

Mwalimu huyo ameachiwa kwa dhamana na polisi hadi Agosti 15. Haikufahamika kama amesimamishwa na shule yake.

Msemaji wa Polisi wa Greater Manchester alisema: "Polisi wa Greater Manchester wanafanya uchunguzi baada ya mwanaume mmoja kuwa amekutwa kwenye chumba cha msichana wa miaka 16.

"Ijumaa, Julai 19, polisi waliitwa sehemu fulani katika eneo la Bolton kufuatia kuhusiana na ustawi wa binti wa miaka 16 ambaye anaishi katika sehemu hiyo.

"Maofisa walifika na baadaye siku hiyo mwanaume mwenye umri wa miaka 35 alikamatwa kwa tuhuma za kukiuka maadili ya nafasi yake.

"Ameachiwa kwa dhamana hadi Agosti 15, mwaka huu akisubiria hatua zaidi.

"Maofisa Polisi wa Greater Manchester na taasisi kadhaa katika eneo la Bolton wanachunguza mazingira yaliyochangia tukio hilo. Uchunguzi huu pia utatazama mambo yoyote ya ulinzi ambayo yanahitaji kujadiliwa na kuona kama kuna makosa yoyote yametendeka."

Tukio hilo limekuja takribani mwezi mmoja baada ya mwalimu wa shule aliyeoa, Jeremy Forrest kufungwa jela miaka mitano na nusu na Mahakama ya Lewes kwa kuteka mtoto mmoja baada ya kutoroka kutoka Ufaransa na mwanafunzi wa miaka 15.

Muathirika wake, sasa miaka 16, ameshikilia msimamo wa kubaki upande wa mtuhumiwa na wawili hao wamepanga kufunga ndoa mara atakapoachiwa kutoka gerezani
.

No comments:

Post a Comment