aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 31, 2013

MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUCHEZA MECHI NYINGI ZA KIMATAIFA - AHMED HASSAN AGHAIRI KUSTAAFU

Mchezaji mwenye rekodi ya kucheza mechi nyingi zaidi za kimataifa. 
Ahmed Hassan, ameamua kutostaafu kwa kuongeza msimu mmoja wa 
kuichezea klabu ya Misri Zamalek.

Kiungo huyo mwenye miaka 38, ambaye kwa sasa amejiuzulu kuichezea 
timu ya taifa ya Misri, atacheza kwenye michuano ya kombe la 
mabingwa wa Afrika nchini, klabuya Cairo ilisema kupitia taarifa
 yake rasmi. 

Huu ni msimu wake wa pili akiwa na Zamalek, ambaye alijiunga 
nayo akitokea kwa mahasimu wao Al Ahly mwaka jana.
Hassan anatambuliwa na shirikisho la soka la kimataifa FIFA kuwa 
ndio mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi za kimataifa, akiwa 
ameiwakilisha Misri mara 184 kuanzia 1995 mpaka 2012. 

Hassan, ambaye ana rekodi ya kushinda kombe la mataifa huru ya 
Afrika mara nne, lakini hajawahi kucheza kwenye michuano ya
 kombe la dunia, pia aliwahi kucheza soka nje ya nchi katika 
klabu ya Anderlecht ya Belgium na Besiktas iya Uturuki.

No comments:

Post a Comment