aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 31, 2013

BAADA YA LIONE MESSI - SASA RAISI WA BAYERN MUNICH ASHTAKIWA KUKWEPA KODI


Wiki kadhaa baada ya mchezaji bora wa dunia Lionel Messi 
kutuhumiwa kukwepa kulipa kodi, sasa raisi wa mabingwa 
wa ulaya Bayern Munich Uli Hoeness ameshatakiwa kwa 
makosa ya kukwepa kodi, mwendesha mashtaka wa
 Ujerumani amethibitisha.

Imegundulika kwamba mnamo April mwaka huu, Uli, 61,
 alishindwa kulipa kodi ya kodi akaunti yake iliyopo 
nchini  Switzerland mnamo mwezi January, na sasa
 imethibitika ameshtakiwa kwa makosa ya kukwepa kodi.

"Mwendesha mashataka wa jiji la Munich II amekamilisha 
uchunguzi," taarifa rasmi ilisema.

"Mahakama ya makosa ya jinai ya mkoa wa Munich II 
sasa inasubiriwa kuamua kukubali au kukataa mashtaka hayo."

Msemaji wa klabu ya Bayern Markus Horwick aliiambia
 SZ kuhusu issue hiyo: "Hatutosema kitu chochote kuhusu suala hili."

No comments:

Post a Comment