aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 31, 2013

MAMA WA JOHN TERRY AKESHA BAA

LONDON, ENGLAND

MAMA mzazi wa beki wa kati wa Chelsea, John Terry, Sue, amekutwa akiwa amelewa chakari na kuuchapa usingizi katika siti ya nyuma ya teksi aliyokodi baada ya kuzidiwa na pombe alizokunywa usiku kucha katika baa moja jijini London.

Mama huyo mwenye umri wa miaka 55, alipanda ndani ya teksi hiyo saa 9 za alfariji akiwa ametoka kuponda raha na mkwewe, mke wa Terry, Toni.
Kwenye teksi hiyo, bibi Sue alitangulia kupanda na kwa sababu alichoka, aliamua kuangusha usingizi katika siti ya nyuma akimsubiri Toni atoke ili warudi nyumbani.
Tukio hilo la ulevi wa mama huyo, limekuja siku chache baada ya baba mzazi wa mwanasoka huyo kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za ubaguzi.

No comments:

Post a Comment