aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 31, 2013

VIONGOZI WAFUNGIWA GHALA LA KOROSHO NA KUMWAGIWA UPUPU MTWARA...


Mmea wa upupu shambani.
Viongozi wa Chama cha Msingi cha Ushirika wa Mazao na Masoko
 Lenganelo na Diwani wa Mchemo, Mshamu Chituta, wamekamatwa na 
wanachama, wakafungiwa katika ghala la korosho na kumwagiwa upupu.

Akizungumzia kisa hicho katika Baraza la Madiwani juzi, Diwani huyo 

alisema wanachama hao walishikwa na hasira mkutanoni, baada ya 
kudanganywa, ndipo walipomkamata  yeye na uongozi wa chama hicho na 
kuwafungia kisha kuwamwagia upupu.
Alitaja wenzake waliopata adhabu hiyo kuwa ni Mwenyekiti wa Chama hicho,

 Hassan Nakuya, Katibu aliyemkumbuka kwa jina moja la Mnali na msaidizi 
wake, Ramadhani Mpanga.
Chituta alisema uongozi wa chama hicho, uliwatangazia wananchi kwenye 

mkutano huo, kuwa Mkuu wa Wilaya ya Newala, Christopher Magalla,
 angekuwapo.
Habari kutoka eneo la tukio, zilieleza kuwa viongozi wa chama hicho

 walitumia jina la Mkuu wa Wilaya kuitisha mkutano wa wanachama, ili 
kuwavuta wahudhurie kwa wingi.
Diwani Mshamu alisema hakuwa anajua kama uongo ulitumika, kwa kuwa

 siku ya tukio alikuwa na kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata, lakini 
aliombwa na Katibu wa Chama cha msingi, asitishe kikao hicho na aende
 kwenye mkutano wa chama ambao pia ungehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya.
Kwa mujibu wa diwani huyo, wanachama waliitika mwito lakini mkutano 

ulianza bila Mkuu wa Wilaya, wakagundua kudanganywa ndipo wakaamua 
kuwaadhibu viongozi na yeye kwa kuwafungia ghalani na kuwamwagia 
upupu.
Alisema walijaribu kuwasiliana na Mkuu wa Wilaya, ili afike kuwanusuru,

 lakini simu yake haikupatikana hivyo wakakaa ghalani kwa saa kadhaa,
 mpaka walipomtafuta  Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD), aliyefika 
kuwafungulia.
Kutokana na malalamiko hayo ya Diwani katika Baraza hilo ambalo Magalla 

pia alihudhuria, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Newala, Ashidi Ndembo, 
alimwomba Mkuu wa Wilaya, kutoa ufafanuzi wa suala hilo, ili kuondoa hali 
ya sintofahamu baina ya diwani na uongozi wa chama cha msingi.
Akijibu hoja hizo, Magalla alisema hakuwa na taarifa na mkutano huo na 

kwamba siku inayotajwa kufanyika mkutano huo, alikuwa kwenye kikao cha
 Kamati ya Ulinzi na Usalama cha Mkoa, mjini Mtwara.
“Nataka nichukue nafasi hii kueleza kwamba sikuwa na taarifa ya mkutano 

huo, siku hiyo nilikuwa katika kikao mjini Mtwara na simu nilizima kutwa 
nzima. Nilipoiwasha, nilikuta ujumbe kutoka kwa mtu nisiyemjua, nilipopiga 
simu nikagundua ni Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Lenganelo,”
 alisema Magalla.
Alisema baada ya kumpigia, Mwenyekiti huyo alimfahamisha kuwa alikuwa 

amefungiwa ghalani na wakulima na alimpigia kutaka msaada lakini simu 

haikupokewa, ingawa walishafunguliwa.
Magalla alionya wanaotumia jina lake kuitisha mikutano ya wananchi kwa 

kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria na utovu wa nidhamu, alitaka 
wahusika wa jambo hilo waache kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa
 dhidi yao.
“Nimesikitishwa sana na kitendo hiki, hasa ninaposikia kinafanywa na 

viongozi wenzangu. Kwa kweli si jambo jema…tunajua kuna baadhi ya 
maeneo wananchi wamekuwa hawajitokezi wanapoitwa katika vikao na 
mikutano, sasa kama viongozi wa eneo hilo wanahitaji msaada wa DC, ni 
vema wakawasiliana nami na kwa kuwa huo ni wajibu wangu nitakuja,” 
alisema Magalla.

No comments:

Post a Comment