aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 31, 2013

Baada ya Watanzania kukamatwa na dawa za kulevya, hiki ndio kimemkuta Madee akiingia Afrika Kusini






1
Kwenye Exclusive interview na millardayo.com 

Madee amehadithia kila kitu kilichomtokea wakati 
anaingia tu Afrika Kusini siku kadhaa zilizopita 
ambapo hii imetokea kutokana na ukubwa wa habari, 
uzito wa tukio la wale Watanzania wawili 
wasichana waliokamatwa kwenye kiwanja 
cha ndege Johannesburg 
wakiwa na dawa za kulevya wakitokea Tanzania.
Madee anakwambia alipotua kwenye kiwanja cha ndege,
 kawaida huwa kuna utaratibu wa kuchekiwa hati ya
 kusafiria na ukaguzi mwingine ambao hufanywa 
na mitambo maalum kwa kila abiria anaeingia 
Afrika kusini, ni ukaguzi ambao unafanywa Airport
 kabla ya abiria kuruhusiwa kuingia kwenye nchi yenyewe.
Kilichomfanya Madee kusachiwa na kuhojiwa karibu
 dakika 60 ni pale tu aliposema anatokea Tanzania, 
kuna wazungu wawili wenye sare tofauti za kipolisi
 wakaanza kumsachi mpaka kufikia kumwambia avue 
t shirt yake, alivua t shirt na kubakiwa na nguo
 nyepesi ya ndani wakati huo abiria wenzake

 aliokwenda nao walikua wameruhusiwa.
Kati ya abiria wote waliokuja pamoja kwenye ndege, 
Madee na Mzimbabwe mmoja ndio walikaguliwa 
sana ila huyo mwingine alikaguliwa kidogo tu kama 
dakika 10 na wala hakuambiwa avue nguo.
Sehemu yenyewe Madee aliyoambiwa avue nguo sio 
kwenye chumba maalum, ni palepale kwenye
 foleni wanaposimama watu ila 
kwa pembeni kidogo, ni 
sehemu ambayo imezibwa na kioo kinacholingana 
na usawa wa tumbo kushuka chini…. Madee 
anakwambia jamaa walinong’onezana sana wakati 
wanamkagua.
Hata hivyo baada ya Askari hao kumuweka sana 
msanii huyu wa bongofleva kutoka kundi la 
TipTop Connection walimuomba radhi baada ya
 kumaliza ukaguzi wao ambao pia ulihusika 

kulivuruga sana begi lake.

2

                                                            SOURCE MILLARD AYO

No comments:

Post a Comment