aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Tuesday, December 17, 2013

WEMA AFUNGA MWAKA KWAKUWEKA PICHA MTANDAONI IKIONYESHA UZURI WA MGONGO WAKE


 Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Sepetu hivi karibuni ameachia picha tata kwenye akaunti yake ya Mtandao wa Instagram zikimuonesha akiwa ameacha mgongo wazi, jambo lililotafsiriwa na wengi kuwa ameamua kufunga mwaka huu kwa staili hiyo ya kuacha mgongo nje, Showbiz inakudondoshea. 
Wema Sepetu akiwa ameacha mgongo wake wazi.
Katika picha hizo, Wema anaonekana kujichora tatoo kibao kuanzia shingoni na kumfanya aonekane tofauti na alivyozoeleka jambo lililofanya wengine wamsifie huku wengine wakimponda mbaya.
“Sasa Wema kujichora hivyo mgongoni ndiyo nini? Bora ungeuacha mgongo wako kama ulivyokuwa zamani,” alichangia mmoja wa wadau na kuungwa mkono na wenzake.
Showbiz ilipomvutia ‘waya’ Wema ili kumuuliza kulikoni ameamua kupiga picha za kuuanika mgongo wake, simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
-GPL 

No comments:

Post a Comment