aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Thursday, December 19, 2013

MWENYEKITI WA SIMBA "ISMAIL RAGE" AKUBALI KUJIUZURU...SOMA ALICHOKISEMA



ragee
Wanachama wa klabu ya Simba wamemjia juu Mwenyekiti wake Ismail Aden Rage juu ya suala zima la mchezaji Emanuel Okwi, 
Hivi ndivyo alivyosema Rage ‘Mimi najiuliza ndo maana nimeomba ufafanuzi toka Fifa baada ya kufika tu,mi nilikua sipo nchini kwa mwezi mzima nimeandika barua kwenda Fifa jana ile ile na pia Tff tumeandika barua kwa niaba ya Simba ili kutoa malalamiko yetu,kwa sababu hata sisi inatuchanganya huyu mchezaji mkataba wake,labda kama kuna ushahidi watuonyeshe kama Fifa wamevunja mkataba na Etoile du Sahel  lakini ukisoma kwenye mtandao wa Fifa kuna kesi 3 ziko pending’.
‘kesi ya Simba kuidai Etoile du Sahel  kuna kesi ya Etoile du Sahel  kulalamika mchezaji wao ametoroka,kuna kesi ya Emanuel Okwi kudai pesa zake hajalipwa na Etoile du Sahel,kwa hiyo huu ujanja uliotumika sijui umetokea wapi tumelalamika Fifa wakati tunamtoa Villa walisema wamempeleka Villa kwa mtaba wa miezi 6 na miezi 6 haijaisha,jana nimeona kwenye luninga  moja wanaonyesha ITC ile ITC kila club Tanzania inawezaa kuprint tu.’
‘Uganda matatizo yao walisaidiwa kutatuliwa kwa haraka na chama chao cha mpira cha Uganda sisi chama chetu hapa lazima niseme ukweli hawajatusaidia vya kutosha wamelala kwa muda mrefu sijui  kwa sasa hivi kwa sababu amekuja  mheshimiwa Malinzi labda wataanza kusaidia vilabu vytu kuhakikisha tunapata haki zetu kwa sababu Fifa wana utaratibu wao wa kuheshimu wanachama wao wanatoa uzito kwa mfano Sector General wa Fifa anaweza kuongea na Sector General wa tff lakini si mimi President wa Simba,siwez kuongea na Sector General wa Fifa moja kwa moja  mi naongea na makanjanja tu’.
‘Kwenye sheria tuna kitu kinaitwa Legal Status Kwa wanachama wa tawi la Mpira Pesa hawana hadhi ya kisheria ya kuongea masuala ya simba maana hao si tawi la simba lililosajiliwa hawana hata hiyo hati na haiwezekani katika matawi 78 tawi 1 tu kila siku wanaongea mi wangeongea matawi 78 kidogo ningeshtuka ,mimi nimechaguliwa na watu 1,820 sasa tawi la mpira pesa sijui lina watu 204 sijui 100 ila hata sielewi lina watu wangapi,haliwezi kunipa taabu’.
‘Sina nia ya kuitisha mkutano wa dharura kama hali itaendelea hivi ya kutoelewana njia nyepesi nayoona ndugu yangu ni kuitisha mkutano wa uchaguzi mwezi January kabla ya tarehhe 27 Januaryili upatikane uongozi mpya  kuanzia Mwenyekiti na wajumbe wa kamati ya utendaji’
‘Napitia vifungu vya sheria nisome na ngojea uamuzi wa Tff watasema nn kuhusu malalamiko yangu,maana baada ya maazimio ya kamati utendaji  niliandika barua kuomba kamati ya utendaji ipitie maamuzi yake ya mwanzo kulikua na dosari nilizona na nikaeleza dosari nilizoziona kwa hiyo wakirekebisha hizo dosari nipo tayari kufata’
‘Mimi binafsi siwezi kufanya kazi na kamati ambayo tayari  ilishanituhumu  na kunisimamisha kwa hiyo tayari hawana imani na mimi sasa mimi imani na wao natoa wapi,kwa hiyo tutakua hatuwatendei haki wanachama wa Simba,sasa ili tuonekane wote tunafata maadili basi ni vyema kuanzia Mwenyekiti na Wajumbe wote wa kamati ya utendaji tukajiuzulu tukaitisha mkutano wa uchaguzi  ili kuikoa klabu yetu ili ipate mafanikio makubwa’.

No comments:

Post a Comment