aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Sunday, December 22, 2013

Sababu ya Tanzania, Afrika Kusini na Zambia kutumia wimbo wa taifa wenye melody inayofanana

 Huenda ukawa umejiuliza swali hili kwa kipindi kirefu lakini hujawahi kupata jibu. Kwanini Tanzania, Afrika Kusini na Zambia zinatumia wimbo wa taifa wenye melody inayofanana?Melody za wimbo huo ambao kwa Tanzania unaitwa ‘Mungu Ibariki Afrika, zimetoka kwenye wimbo uitwao “Nkosi Sikelel’ iAfrika”, neno la lugha ya Xhosa lenye maana hiyo hiyo pia). Wimbo huo ulitungwa mwaka 1897 na Enoch Sontonga, aliyekuwa mwalimu kwenye shule ya misheni ya jijini Johannesburg.

Wimbo huo ulianza kutumika kama wimbo maalum wa hekaheka za ukombozi wa Afrika na baadaye kuanza kutumiwa kama nyimbo za taifa za nchi tano barani Afrika, zikiwemo Zambia, Tanzania, Namibia na Zimbabwe baada ya kupata uhuru.

Zimbabwe na Namibia zimepata nyimbo zingine za taifa. Wimbo huo kwa sasa unatumika Tanzania, Zambia na tangu mwaka 1994 kama sehemu ya wimbo wa taifa wa Afrika Kusini.
Hata hivyo ikumbukwe kuwa Tanzania ndio ilikuwa nchi ya kwanza kuanza kuutumia wimbo huo kama wimbo wa taifa 1961 pale ilipokuwa Tanganyika na kuendelea nao baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964

Tafsiri ya mashairi ya awali yaliyokuwa kwa lugha Xhosa kwenda Kiswahili ilifanya na kundi la watu.
Wimbo unaotumiwa na Afrika Kusini hata hivyo ni mchanganyiko wa “Nkosi Sikelel’ iAfrika” na “The Call of South Africa” (unaojulikana kwa lugha ya Afrikaan kama “Die Stem van Suid Afrika”).

20 April, 1994 ndipo ilipotangazwa kwamba zote Nkosi Sikelel’ iAfrika na Die Stem ziwe nyimbo za taifa za Afrika Kusini. Wimbo uliounganishwa ulianza kufanya kazi October, 1997, 

baada ya maneno ya Kiingereza yalipoongezwa na wimbo kupangwa upya na Jeanne Rudolph. 

No comments:

Post a Comment