aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Tuesday, December 24, 2013

HOME DR SLAA AMPIGA MARUFUKU ZITO KUFANYA MIKUTANO,NI BAADA YA ZITO KUFUNIKA KATIKA MIKUTANO HIYO



Zitto Kabwe jana  amefanya mkutano wa 3 ndani  ya Mkoa wa Kigoma,mikutano hii  ilianza siku ya Jumamosi kwa  sehemu ya Mwandiga mahali alipozaliwa na kukulia,Kasulu ilikua juzi  na jana kafanya Kigoma mjini eneo la Mwanga kwenye uwanja wa Community Centre....
 
Mkutano ulianza sa 10 kiitifaki ulitanguliwa na viongozi wa Chadema wa mkoa,kisha Zitto Kabwe kupanda Jukwaani na moja kati ya vitu alivyovizungumzia ni kuhusu tamko la Dr.Wilbroad Slaa alipokuwa kwenye mkutano wake  wa Kuimarisha chama uliofanyika Igunga Mkoani Tabora....
 
Dr.Slaa alizungumzia kuhusu mikutano anayoifanya Zitto Kabwe kuwa si halali yeye anatakiwa kufanya kwenye jimbo lake tu ambalo ni Kigoma Kaskazini .
 
Hiki ndicho alichokizungumza kufuatia tamko hilo la Dr.Slaa  "Sasa jana (juzi ) Katibu Mkuu kasema Kwanini nafanya ziara zaidi ya Kigoma Kaskazini siruhusiwi kwenda sehemu nyingine yoyote baada ya kusikia yale mapokezi ya Kasulu.
 
"Mimi nawaambia katiba ya Nchi hii inaniruhusu kwenda mahali kokote,sehemu yoyote nchi hii kwa mujibu wa katiba maana mimi bado ni Mbunge.Kama wamenifukuza waseme kuwa wamenifukuza lakini kama hawajanifukuza mimi bado mbunge"
 
"Kwa hiyo nitaenda Kigoma Kaskazini,nitaenda Kigoma Kusini,nitaenda Kasulu,nitaenda Kigoma Mjini kuhutubia Wananchi na siyo hivyo tu nitaenda Mpanda,nitaenda Tabora,nitaenda Shinyanga,nitaenda Mwanza nitaenda hadi Arusha na hakuna mtu wa kunizuia."
Add caption
 
 
 

No comments:

Post a Comment