aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, January 20, 2014

WENYE PESA:USICHOKIFAHAMU KUHUSU MATAJIRI WAKUBWA KUTOKA TANZANIA... MFAHAMU 'BAKHRESA' NA MATAJIRI WENZAKE 10 WA TANZANIA


  
Said Salim Awadh Bakhresa.
 
KATI ya miaka ya 1960 hadi 1980, mtu kuwa tajiri alionekana ni hatari kwa taifa, tena mali zake alizimiliki kwa kificho, vinginevyo angeitwa mhujumu uchumi. Lakini kwa sasa mambo yamebadilika, taratibu sera za kibepari zinatawala, ujamaa unapewa kisogo.
Mtu kama ni mbunifu, ana nidhamu ya kutofuja pesa na anafanya kazi sana kwa nini asiwe tajiri? Utandawazi unasaidia ndiyo maana leo tunaweza kuwatambua mabilionea wakubwa ambao wanastahili pongezi kwa hatua walizopiga. Tusisahau kuwa wanaibeba nchi kwa ulipaji kodi.
 1. SAID BAKHRESA
Jina lake kamili ni Said Salim Awadh Bakhresa. Jarida la Forbes mwaka jana, lilimuorodhesha miongoni mwa matajiri 40 Afrika kwamba anamiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 620 (karibu shilingi trilioni moja). Hata hivyo, inadaiwa kuwa tabia ya usiri wa Bakhresa inafanya mali zake zisijulikane sana, ila ni tajiri zaidi ya kiwango hicho.
Ndiye mmiliki wa makampuni ya Bakhresa yanayotoa bidhaa zenye chapa ya Azam ambazo zinauzwa nchi mbalimbali Afrika. Ana viwanda vya nafaka na vinywaji, vyombo vya usafiri wa majini, uuzaji wa chakula, bidhaa za plastiki na kadhalika. Ndiye mmiliki wa Klabu ya Azam FC.

2. GULAM DEWJI

Huyu ni baba wa mfanyabiashara maarufu nchini, Mohamed Dewji ‘Mo’. Jarida la Forbes mwaka jana lilimtaja kuwa na utajiri wenye thamani ya dola milioni 560 (karibu shilingi bilioni 900). Mafanikio yake kibiashara yalianza mwaka 1970. Kiwanda chake cha 21st Century Textiles, kinatajwa kuwa moja ya viwanda vikubwa vya nguo Afrika.

3. ROSTAM AZIZ
Inadaiwa anamiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 420 (shilingi bilioni 672). Anamiliki karibu asilimia 40 ya hisa Kampuni ya Vodacom Tanzania. Ni mmiliki wa Kampuni ya Caspian inayohusika na uchimbaji wa madini na ukandarasi nchini Tanzania, nchi kadhaa za Afrika na Asia.

4. DK. REGINALD MENGI
Anatajwa kumiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 280 (karibu shilingi bilioni 450). Ni mmiliki wa kundi la makampuni ya IPP, yanayomiliki vyombo vya habari, viwanda, migodi ya dhahabu, Tanzanite na kadhalika.

5. ALI MUFURUKI
Utajiri wake unatajwa kuwa na thamani ya dola milioni 110 (shilingi bilioni 176). Ni mmiliki wa kundi la makumpuni ya Infortech Investment, inayomiliki maduka yanayouza vitu vya rejareja Tanzania na Uganda. Vilevile ana vitega uchumi vingine. 

6. MUSTAFA SABODO
Ni mfayabiashara mkubwa sana nchini anayemwaga mamilioni kwa misaada. Wakati wa kuanzishwa kwake, aliipa Taasisi ya Mwalimu Nyerere shilingi milioni 800, akasaidia shilingi milioni 100 katika mradi wa kustawisha mimea jamii ya kunde. Vilevile alikipa Chadema shilingi milioni 300. Inadaiwa kuwa utajiri wake unazidi shilingi bilioni 100. Kampuni yake ya Khoja Shia Itnasheri Jamat (KSIJ), ndiyo yeye tenda ya kujenga maeneo ya maegesho ya magari Posta, Dar esSalaam, mradi wenye thamani ya shilingi bilioni 5.6.

7. ABDUL-AZIZ ABOOD

Kiwango chake cha utajiri hakiwekwi sana wazi lakini anatajwa kuwa miongoni mwa mabilionea 10 wanaotikisa nchi kwa sasa. Anamiliki viwanda kadhaa mkoani Morogoro, vyombo vya habari, Abood Radio na TV. Anamiliki mabasi ambayo yanafanya safari zake kati ya Morogoro, Mbeya na Dar es Salaam. Ni Mbunge wa Morogoro Mjini (CCM).

8. MICHAEL SHIRIMA
Ni mmiliki mkuu wa Shirika la Ndege la Precision ambalo linafaya safari zake ndani ya Tanzania pamoja na nchi mbalimbali za Afrika. Ana asilimia tano ya hisa katika Beki ya I&M (Tanzania), vilevile ni memba katika bodi ya wakurugenzi wa benki hiyo yenye thamani ta shilingi bilioni 200. Hisa zake Precision ni asilimia 42.91.

9. YUSUF MANJI
Kiwango halisi cha utajiri wake bado hakifahamiki lakini anafahamika kama mmoja wa mabilionea wakubwa nchini Tanzania. Ni mmiliki wa makampuni ya Quality Group na majengo ya Quality Centre, Quality Plaza na kadhalika. Ni Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga na utajiri wake umeifaya timu kutotetereka tangu alipoanza kuiongoza.

10. MOHAMMED DEWJI
Baba yake anashika nafasi ya pili katika orodha hii. Dewji au Mo kama anavyoitwa na wengi, anatajwa kuwa bilionea nambari moja katika orodha ya mabilionea vijana Afrika (orodha hiyo tuliitoa wiki iliyopita). Ni mmiliki wa makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL) ambayo inatengeneza faida ya shilingi bilioni 136 kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment