aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Thursday, January 16, 2014

PICHA:DAMPO JIPYA LA KISASA LA KUTUPIA TAKATAKA LINALOJENGWA JIJINI MBEYA


Huu ndiyo muonekano wa dampo hilo la kisasa kwa upande wa juu ambapo ujenzi upo katika hatua za mwishoni.
 Hili ni eneo ambapo magari yaliyobeba takataka yatakuwa yanaingia na kumwaga takataka hizo.
 Muonekano wa karibu wa ndani wa dampo hilo la kisasa jijini Mbeya.
 Chemba pekee ambayo ni maalum kwa ajili ya kupitishia takataka zenye kimiminika, pia kupitishia takataka ambazo zitakuwa zimesagwa na kupelekwa katika bwawa maalum litakalotumika kutengenezea umeme pamoja na mabaki mengine ya takataka yatatumika kutengenezea mbolea.
 Hapa ndipo takataka hizo zitakuwa zikitelemkia.
Dampo hilo la kisasa kwa ndani ambapo kwa sasa wameweka kokoto ndogondogo chini  huku ujenzi ukiendelea.
 Kingo pembezoni mwa dampo hilo.
 Hii ni sehemu maalum ambayo itajengwa kisasa kwa ajili ya kuoshea magari baada ya kumwaga takataka.
Hii ni sehemu ya kupaki magari ambayo yatakuwa yakitupa takataka katika dampo hilo la kisasa.

HIVI NDIVYO TAKATAKA ZILIVYOKUWA ZIKITUPWA KABLA YA DAMPO HILO KUJENGWA KATIKA ENEO HILO
Pichani ni jinsi takataka kutoka pande mbalimbali za jiji la Mbeya zilivyokuwa zikitupwa kabla ya dampo hilo la kisasa kujengwa katika eneo hilo jirani na mlima Nyoka jijini Mbeya. Dampo hilo la kisasa linategemea kuanza kufanya kazi hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment