aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, August 5, 2013

HUDUMA YA UTOAJI WA TAARIFA ZA WAHAMIAJI HARAMU UMEZINDULIWA LEO HII JIJINI DAR ES SALAAM

\


Watanzania wametakiwa kuitumia vema huduma mpya ya utoaji taarifa za 

wahamiaji haramu pamoja na taarifa za waathirika wa biashara hiyo, ili kupata 
msaada na kupunguza kasi ya biashara hiyo nchini.
Huduma hiyo imezinduliwa leo jijini Dar es Salaam na shirika la kimatiafa la 

Wahamiaji (IOM) kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani, ambapo 
Mkurugenzi 
wa Sera na Mipango wa Wizara hiyo, Haji Janabi ametoa wito wa matumizi sahihi ya 
huduma hiyo katika kutoa taarifa za wahamiaji haramu pamoja na vitendo vya biashara 
haramu ya binadamu.
Huduma hiyo ambayo ni kitabu chenye namba za simu za vyombo mbalimbali, vikiwemo

 vyombo vya dola vinavyotoa msaada wa haraka, imekuja wakati ambapo Tanzania
 imekuwa ikishuhudia ongezeko la matukio ya wahamiaji pamoja na biashara 
haramu ya binadamu.

No comments:

Post a Comment