aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Sunday, June 15, 2014

WEMA SEPETU ADAKA MIMBA YA DIAMOND


'Beautiful  Onyinye'  na  kipenzi  cha  Diamond, Wema  Sepetu  sasa  ni  mjamzito. Baada  ya  misukosuko  ya  muda  mrefu  ikiwemo  kuporwa  na  wasichana  wenzake  penzi  lake  la  Diamond, sasa  Wema  amepata  kile  alichokuwa  akikililia  kwa  muda  mrefu....

Chanzo  cha  habari  hii  kutoka  kwa  marafiki  wa  Diamond  kimedai  kuwa  Wema  amenasa  ujauzito  na  kugundulika  hivyo  walipokuwa  Afrika  Kusini  kwenye   tuzo  za  MTV-MAMA na  kumfanya  Diamond  achanganyikiwe  kwa  furaha....

Kwa  mujibu  wa  chanzo  hicho, inadaiwa  kuwa  Diamond  kwa  sasa  kawa  kama  mtu  aliyepagawa  kwa  furaha  kutokana  na  taarifa  hizo  njema  na  tayari  ameshaanza  maandalizi  ya  kijacho  chake....

Kugundulika  kwa  ujauzito  wa  Wema  ni  baada  ya  kuanza  kujisikia  vibaya  walipokuwa  Afrika  Kusini  ikiwemo  kichefuchefu  na  kizunguzungu  alipokuwa  hotelini  alipofikia  na  kulazimika  kwenda  hospitali  kwa  uchunguzi  zaidi....

Inasemekana  kuwa  Wema  alisindikizwa  na  Aunt  Ezekiel  kwenda  hospitalini  waliyekuwa  naye  huko  Afrika  Kusini  kumpa  sapoti  Diamond  na  madaktari  ndiyo  waliomjuza  kuwa  anakiumbe  tumboni  cha  wiki 7...

Taarifa  za  madaktari  hao  zilimfanya  Wema  awe  kama  mwehu  aliyepagawa  na  kurudi  hotelini  kwa  mumewe  Diamond  huku  akiwa  na  tabasamu  ambalo  hapo  awali  Diamond  hakuwahi  kuliona....


Inasemekana  kuwa  mpaka  sasa  siyo  Diamond  wala  Wema  aliyewaambia   wazazi  wake  kuhusiana  na  mimba  hiyo  zaidi  ya  watu  wa  karibu  wa  wawili  hao  waliowasindikiza  Afrika  Kusini.

No comments:

Post a Comment