aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Wednesday, June 11, 2014

MREMBO ATEMBEA UCHI MBELE YA UMATI WA WATU..SINZA AFRIKA SANA


...AKIWA CHINI NIDO NJE.  

 ...Akizua timbwili kwa wananchi waliokuwa eneo hilo. 
TIMBWILI! Mrembo wa haja ambaye jina halikupatikana mara moja, amenaswa akiwa matiti ‘nido’ nje baada ya kulewa tilalila mchana kweupe na kulizwa mkoba wake kisha kuzua varangati ‘hevi’, Ijumaa Wikenda lina mkanda kamili.



Mrembo akidhibitiwa baada ya kuzua timbwili.
Varangati hilo lililonaswa na kachero wetu aliyekuwa kwenye ‘patroo’ yaOparesheni Fichua Maovu (OFM), lilijiri wikiendi iliyopita maeneo ya Sinza-Afrika Sana jijini Dar.

Katika sinema hiyo ya bure, mrembo huyo alishuhudiwa akipigana na kila mtu aliyekutana naye mbele yake huku akivua nguo kuashiria kuwa ‘pombe si chai’.
 
..Akitulizwa na wananchi. Kuna wakati mwanadada huyo alikatiza barabarani bila kujali magari na nusura agongwe jambo lililosababisha mtafaruku wa foleni huku mwenyewe akidondoka kama ‘embe dodo’ lililoiva.



...Akionyesha kutokubaliana nao na kuzidi kukinukisha.
Baada ya timbwili hilo kuchukua takriban dakika 35, ilibidi wasamaria wema kuingilia kati na kumshika huku akiwapiga baada ya kuona huenda angeumizwa.

Baadaye watu hao walifanikiwa kumtoa eneo la barabara huku wakimsitiri kwa kupandisha nguo kufunika nido kisha kumpeleka pembeni na kumtuliza. 
“Kweli pombe siyo chai. Yaani msichana mzuri lakini ona alivyojidhalilisha,” alisema mmoja wa mashuhuda hao.
  ...Akiondoka huku nido zake zikiwa wazi.
Paparazi wetu alitaka kujua kulikoni kuwa katika hali hiyo ambapo mrembo huyo alijibu kwa kifupi kuwa kuna mtu alimuibia mkoba wake hivyo akawa hana namna nyingine zaidi ya kufanya fujo kutokana na hasira.

No comments:

Post a Comment