aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, September 2, 2013

"CUF NI CHAMA CHA ZANZIBAR"....TUNDU LISU

Mbunge wa Singida Mashariki mh Tundu Lissu,amesema kuwa CUF ni chama cha Zanzibar. Akizungumza kipitia Star tv ktk kipindi kiitwacho MEDANI ZA SIASA NA UCHUMI.
 
Akihojiwa na mtangazaji wa star tv amesema kuwa hakuna haja ya kutafuta ushahidi kuhusu hilo kwani tangia kuanzishwa kwa vyama vingi nchini Tanzania CUF haijawahi kupata wabunge zaidi ya 3 wa kuchaguliwa huku bara. Hii inaonyesha wazi kwamba CUF ngome yake ni Zanzibar.
 
Akiulizwa kuhusu CDM kuwa kutokuwa na Wabunge Zanzibar,alijibu kuwa ni kweli ila ukweli ni kuwa uweze kushinda uchaguzi Tanzania huitaji kushinda Zanzibar. Kwanza Zanzibar haina hata kura milioni moja zaidi sana ni kura laki tano,na Jimbo la Ubunge pekee lina zaidi ya kura laki nne.
 
Huyo ndie Tundu Lissu Mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani Bungeni. Je yawezekana ni kweli CUF ni chama cha Zanzibar?


SOURCE:GLJ

No comments:

Post a Comment