aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Saturday, September 28, 2013

MAKUNDI YA KIGAIDI YAPANGA KUVAMIA FAINALI ZA MISS WORLD 2013 AMBAYO YAMEPANGWA KUFANYIKA NCHINI INDONESIA..!!


 
Hali ya usalama katika kisiwa cha Bali nchini Indonesia ambako shindano la Miss World 2013 litafanyika Jumamosi hii, imeendelea kuwa hatiani kutokana na vitisho kutoka kwa wanaharakati wa dini ya Kiislamu wanaotishia kulishambulia.
 000_hkg8989120.siWanawake wa Kiislamu wakiandamana dhidi ya shindano ka Miss World huko Banda Aceh, kwenye kisiwa cha Kaskazini cha Sumatra, September 14, 2013

 Kutokana na Indonesia kuwa nchi yenye Waislamu wengi duniani, waandaaji wa shindano hilo walilazimika kulihamisha kutoka kwenye mji mkuu, Jakarta hadi kisiwani Bali. 

Lakini hata hivyo mambo hayajapoa bado na wanaharakati hao wamepanga kufanya maandamano mengine Jumamosi na kuvunja vizuizi vya ulinzi mkali kwenye shindano hilo.
 1375084_10151957434219974_1998112413_n
 Zaidi ya asilimia 90 ya watu milioni 240 wa nchini humo ni waislamu.
  
 Waislamu wanapinga shindano hilo kufanyika nchini mwao nawakiliita shindano hilo kama la ngono na umal*ya. Pamoja na waandaaji wa shindano hilo ambao makazi yao ni Uingereza kuahidi kulioandoa shindano la bikini na washiriki kuvaa nguo zinazoziba mwili, waandamanaji hao hawakuridhika na kuendelea kuwataka walipeleke kwingine.
 1377298_10151957436454974_1137514725_n
 Mapema mwaka huu, mamia wa wanaharakati wa kundi la Islamic Defenders Front walijaribu kuvamia kisiwani Bali lakini polisi walikabiliana na kundi hilo na kulizuia kupanda ferry ya kwenda kisiwani humo.
  
 Balozi za Marekani, Uingereza na Australia tayari zimeonya kuwa wanaharakati hao wanaweza kulishambulia shindano hilo na kukumbushia tukio la Jihad la ulipuaji wa bomu mwaka 2012 lililosababisha vifo vya watu 200.
  
 Mwaka jana, Lady Gaga aliahirisha concert yake mjini Jakarta baada ya kuzuka maandamano kama hayo kuipinga na kumuita ‘mjumbe wa shetani’ anayevaa sidiria na chupi tu. 

Islamic Defenders Front walitishia kumzuia Lady Gaga asishuke kutoka kwenye ndege na wangeuchoma ukumbi ambako diva huyo wa “Poker Face” angetumbuiza.
  
 Zaidi ya warembo 129 duniani watashiriki kwenye fainali ya Miss World 2013 ambapo Tanzania inawakilishwa na Brigitte Alfred. Zaidi ya walinzi 700 watakuwa wakifanya doria kwenye eneo la tukio kuhakikisha usalama wa washiriki na wageni.

No comments:

Post a Comment