aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, July 7, 2014

Uyu demu wa Balotelli mkali sana aseee


Close embrace: The pair share an intimate moment on their holiday in Miami
Mahaba matamu: Wawili hao walikula raja sana mjini Miami
BAADA ya matokeo mabaya katika Kombe la Dunia akiwa na timu yake ya taifa, Italia, mshambuliaji Mario Balotelli amepigwa picha akivuta sigara na kufanya matanuzi na mpenzi wake Fanny Neguesha mjini Miami, Marekani.
Mshambuliaji huyo wa Milan, ambaye alipigwa faini na klabu yake kwa kuvuta sigara kwenye treni mwaka jana, haonekani kabisa kuwa na dalili za kuacha sigara baada ya kupigwa picha akiwa kwenye korido la hoteli anavuta.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 yupo mapumzikoni na mpenzi wake, Fanny Neguesha baada ya Kombe la Dunia ambako alifunga bao moja tu dhidi ya England, Italia ikitolewa hatua ya makundi.
Maisha ufukweni: Nyota wa Italia, Mario Balotelli akiwa na mpenzi wake Fanny Neguesha mjini Miami
Lighting up: Balotelli was caught smoking on his hotel balcony while on holiday in Miami
Kitu laini: Balotelli akivuta sigara kwa hisia kali mjini Miami
Pick me up: The footballer and his fiance couldn't keep their hands off each other in the water
Niinue baba: Balotelli akiwa amembeba mpenzi wake baharini
Akiwa mapumzikoni, Balotelli pia aliposti picha akiwa na mkanda wa ubingwa wa dunia wa UFC World katika akaunti yake ya Instagram.
Mtaliano huyo awali alisema kwamba kama asingekuwa mwanasoka, angeibukia kwenye mchezo wa sanaa za mapigano.
Balotelli anafikiriwa yuko njiani kuondoka Milan, ambako alitua miezi 18 iliyopita akitokea Manchester City
Fighter: Balotelli also posted a picture with the UFC World Championship belt to social media site Instagram
Balotelli akiwa na mkanda wa ubingwa wa UFC
Support: The Milan striker poses with fans who take a selfie on the beach while on holiday in Florida
Balotelli akiwa na mashabiki wake katika ufukwe mjini in Florida
Milan iko tayari kumuuza mshambuliaji huyo ili kupunguza bajeti yao ya mishahara, huku Arsenal ikiwa miongoni mwa klabu zinazomtaka. 
Balotelli anataka kurudi Ligi Kuu ya England, lakini kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amekanusha kuwa na mpango wa kumsaini mshambuliaji huyo.

No comments:

Post a Comment