aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Sunday, July 20, 2014

AUNT EZEKIEL ASEMA SIJAWAHI MVULIA NGUO DIAMOND NA KUFANYA MAPENZI NAE NA WALA SIFIKIRII KUMTONGOZA....


Wakati  ikidaiwa  kuwa  mwanadada  Aunt  Ezekiel  anamzunguka  Wema  Sepetu  na  kula  Penzi  la  shemeji  yake  Diamond, sasa  ameamua  kufunguka  na  kudai  kuwa  kamwe  hawezi  kumsaliti  Wema  na  kikubwa  anachokiheshimu  ni  kwamba  anajua  Diamond  ni  mpenzi  wa  ndugu  yake.....

Aunt  alisema  hajawahi  kulala  na  Diamond, wala  kumuomba  kutoka   kimapenzi  kama  watu  wanavyodhani  bali  wao  ni  marafiki  wa  karibu  kwani  anatambua  kuwa  Wema  anampenda  Diamond, na  ndio  maana  wakati  wote  wanakuwa  pamoja  na  si  kwamba  yeye  ana lengo  la  kuchukua  nafasi  hiyo.....

"Mimi  jamani  sijawahi  kutoka  na  Diamond  na  wala  sina  lengo  hilo,najua  yeye  ni  shemeji  yangu  kwa  Wema,sasa  inakuwaje  na  mimi  nijipeleke  wakati  najua  kinachoendelea?

"Hayo  mambo  siwezi  kufanya  na  ninachohitaji  kuwaambia  mashabiki  wangu  ni  kwamba  kila  mmoja  ana  mpenzi  wake  na  hatuwezi  kuibiana  wanaume  kama  inavyodhaniwa,"  alisema  Aunt.


Hata  hivyo  alisema kuwa  safari  zote  wanazokuwa  pamoja  ni  jibu  tosha  na  kama  angetaka  kufanya  hivyo  ni  wazi  wangegombana  na  rafiki  yake, kitu  ambacho  hataki  kiwe  hivyo.

No comments:

Post a Comment