aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Tuesday, July 22, 2014

SOMA KIFO CHA SOKOINE KILIVYOTOKEA

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Moringe  Sokoine (kulia) enzi za uhai wake akiwa na Mwalimu Nyerere.
WAZIRI Mkuu (sasa ni marehemu) Edward Moringe  Sokoine alikuwa Dodoma kwenye kikao cha Bunge akiwa ni kiongozi wa shughuli za serikali na alimaliza kikao chake Aprili 11, 1984.
Aliandaliwa usafiri wa ndege ili asafiri na ujumbe wake wakati wa kurejea Dar es Salaam kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa lakini alikataa.
Safari hii sitaki kurudi Dar es Salaam kwa ndege, nataka kurudi kwa gari ili nione hali ya mazao ya wakulima njiani,” alikaririwa afisa mmoja wa Ikulu akimkariri Waziri Mkuu Sokoine mara baada ya kujulishwa habari ya usafiri wa kumrejesha Dar.
Aprili 12, 1984 msafara wake ulianza akitokea Dodoma huku ukisindikizwa na magari ya polisi na wana usalama wa taifa.
Msafara wake mchana ulipofika eneo la Wami mkoani Morogoro, jirani na palipojengwa makao makuu ya sasa ya Wilaya ya Mvomero, gari yake ilipata ajali kwa kugongwa na gari lingine aina ya Toyota Land  Cruiser.
Gari hilo lilikuwa likiendeshwa  na mkimbizi, raia wa Afika Kusini ambaye jina lake ni Dumisani Dube aliyekuwa anaishi kwenye kambi ya wanachama wa chama cha kupigania uhuru wa nchi hiyo cha African National Congress (ANC), Dakawa, Morogoro.
Sokoine alipofikishwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, madaktari walithibitisha kifo chake.
Rais (wa wakati huo), Mwalimu Julius Kambarage Nyerere siku hiyo majira ya jioni alilitangazia taifa kifo cha waziri mkuu wao. Mwalimu Nyerere, alishindwa kuhutubia kutokana na majonzi aliyokuwa nayo.
Dumisani alishitakiwa mahakamani lakini kesi yake haikuendelea (bila shaka kwa sababu za kisiasa), aliachiwa huru lakini alirudishwa kwao Afrika Kusini.
Miaka kumi baada ya kifo chache, daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Sokoine baada ya kifo, aliweka wazi taarifa ya chanzo cha kifo chake.
Sehemu ya taarifa hiyo ilisema kuwa baada ya ajali, Sokoine alivunjika shingo ambayo ilisababisha kubana mishipa ya fahamu (spinal cord) ambayo ilikata mawasiliano kati ya ubongo na sehemu nyingine za mwili.
Kabla ya kifo chake, Sokoine alikuwa pia Mbunge wa Jimbo la Monduli na mwili wake ulizikwa huko kwa heshima zote za kiserikali, japokuwa mila za Kimasai pia zilipewa nafasi katika mazishi hayo.
Mahali alipopatia ajali Sokoine mara baada ya ajali hiyo panaitwa Wami Sokoine na pamejengwa mnara

No comments:

Post a Comment