aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Sunday, July 13, 2014

MAMA DIAMOND AZUNGUMZIA MAISHA YA MWANAE, JINSI WANAWAKE WANAVYOMSUMBUA, PIA AMTAJA MKWE AMPEDAYE KATI YA WEMA NA PENNY! SOMA HAPA

diamond na mama
Mama mzazi wa star anayeipeperusha vizuri bendera ya Tanzania kimataifa kwa sasa kupitia muziki, Nasib Abdul a.k.a Diamond Platnumz jana (July 11) alipata nafasi ya kuzungumza na paparazi, mambo mbalimbali yanayomhusu mwanaye.

Haya ni baadhi ya maswali ambayo aliulizwa na paparazi, pamoja na majibu aliyoyatoa:

Kuhusu tuhuma za Diamond kujihusisha na ushirikina katika muziki wake:
“Hiyo si kweli na wala hana ushirikina, si unajua tena mtu ukiwa juu kila mtu atakusingizia anachowaza yeye ili apate sifa ajulikane…Havijatokea watu uzushi tu wanapenda sasa ushirikina wa nini , kama mtu upo juu upo juu kama upo chini upo chini, nay eye sasa hivi ni nafasi yake kama sio nafasai yake atashuka walikuwepo wangapi, alikuwepo Mr Nice alikuwepo juu, lakini zamu yake imefika imeshuka imekuja zamu ya Nasib wacha awe juu itakapofika yake kushuka atashuka”.

Na hii tabia ya mara (msichana) huyu mara huyu wewe ukiwa kama mama kwako huo unaipokea vipi?
“ Siipokei vizuri laikini sasa nitafanya nini nay eye star, wengine wanajitongozesha bila kutongozwa..mi mwenyewe hapa kutwa napigiwa simu mpaka nazima, wananipigia simu wanafikiria Nasib wanajitongozesha mpaka nawatumia meseji mbona mnajitongozesha, hii sio namba ya Nasib hii namba katoa ya biashara ya Tshirt 0716186318 sio namba ya Diamond, namba yake mama yake.sitaki usumbufu..wananitumia mapicha ya uchi , mapicha ya nini sasa ni ustarabu gani huo”

Yanasemwa mengi kuhusu mahusiano ya Diamond na Wema mara tunasikia kuna Penny…lakini katika habari za pembeni za wadaku watu wanasema mama yake Diamond anampenda zaidi Penny, hilo liukweli mama?
“Mimi sina ninayemchukia, kwasababu mimi mama na mimi nina mtoto wangu wa kiume, akiniletea mkwe siwezi kumkataa, yeye ni wa kiume na lijal, je angekuwa nanii (shoga) mi ningeletewa mwanamke? Nisingeletewa, sasa watu wanavyosema hivyo sijui nampenda nani si kweli mi yeyote anayekuja mi nampenda siwezi kumchukia mtu wote binadamu wenzangu”.

Kwasababu umeishi na Penny na Wema kwa muda wote, Penny ni msichana wa aina gani na wema ni msichana wa aina gani?
Mi navyoona wote sawa kwasababu wananionesha mapenzi wote wananipenda, siwezi kusema nimchukie Penny mtoto wa watu siwezi kumchukia, alikuwa ananionesha upendo unajua tu tena ni ibilisi mwenyewe manake mambo yao mi siwezi kuingilia, lakini wote naona wananipenda.

Wewe unavyoona mama Diamond muda wa kuoa umefika ama bado?
“Umefika lakini mwenyewe bado hajaamua, namwambia lakini mwenyewe anakwambia bado mama, nahitaji mkwe nahitaji mjukuusi unajua tena, nataka mtoto kumwona bado nanguvu zangu nikishakuwa kizeesiwezi kumlea”

Unatamani Diamond aoe mwanamke wa aina gani?
Sasa hayo ni maamuzi yake siwezi kumpangia mwanamke ila napenda mtu awe na nidhamu , anajali familia yake na familia ya kiumeni, sio mwanamke mapepe anajijali mwenyewe hamna, mtu unapokuja sehemu penda familia ukipenda …. upende na…. habari ndio hiyo.

No comments:

Post a Comment