aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Thursday, August 15, 2013

MJADALA: WENGER KAUZA/KATOA MKOPO WACHEZAJI 17 KWENYE DIRISHA LA USAJILI - ARTETA NJE WIKI 6 - ABAKIA NA WACHEZAJI 10 TU WA KIKOSI CHA WALIO FITI KUCHEZA. NINI ANAWAZA KOCHA HUYU?

 Ligi kuu ya England inaanza wikiendi hii - huku timu kubwa baadhi zikiwa zimejipanga vizuri hasa Chelsea. Man City, Liverpool na Spurs, lakini Manchester United na Arsenal hawajawa active kwenye dirisha la usajili hili. Man United wana afadhali kwa sababu wana kikosi chao kile kile walichoshinda nacho ubingwa msimu uliopita. Lakini upande wa Arsenal hali sio nzuri. Mpaka kufikia leo Ijumaa kocha wa timu hiyo Arsene Wenger amesajili mchezaji mmoja tu tena alikuwa huru - Sanogo, huku akiwa tayari ameuza au kutoa kwa mkopo wachezaji 17 wakiwemo mastaa kama Gervinho, Arshavin, Santos, Djorou na wengineo. 

Arsenal mpaka sasa ilikuwa imebakiwa na wachezaji 11 wale wazoefu wa kikosi cha kwanza lakini ghafla usiku wa jana ikatoka taarifa kwamba Kiungo tegemezi Mikael Arteta amepata majeruhi ambayo yatamuweka nje kwa wiki sita za mwanzo mwa msimu wa ligi, hivyo kuiacha Arsenal ikiwa na imebakia na wazoefu 10 tu ambao wanaweza wakaanza kwenye wa kwanza wa ligi dhidi ya Aston Villa.
Wenger amekuwa mtu wa kuzungumza zaidi kuliko utendaji kwenye soko la usajili na siku za dirisha la usajili zinakaribia kuisha.

Kwa hali ilivyo kama Wenger hatokuwa mjanja Arsenal wanaweza wakaanza vibaya ligi. Wenger anawaza nini? Jadili................................


WACHEZAJI WA ARSENAL WALIOBAKI WA KIKOSI CHA KWANZA

Goalkeepers: Szczesny, Fabianski.
Defenders: Mertesacker, Koscielny, Jenkinson, Gibbs, Vermaelen (majeruhi),Monreal (majeruhi), Sagna (majeruhi).
Midfielders: Rosicky, Oxlade-Chamberlain, Wilshere, Ramsey (hayupo fiti)Cazorla (ametoka kusafiri kutoka ECUADOR jana), Arteta (majeruhi)Diaby (majeruhi),Frimpong*, Miyaichi (majeruhi).
Forwards: Podolski, Giroud, Walcott, Sanogo (majeruhi), Park*, Bendtner*.

No comments:

Post a Comment