aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, August 5, 2013

NEYMAR ANAUGUA UGONJWA WA UPUNGUFU WA CHEMBE HAI NYEKUNDU ZA DAMU MWILINI - BARCELONA YATHIBITISHA


Barcelona imesema kwamba mshambuliaji wake mpya kutoka Brazil 
Neymar ameanza kuugua ugonjwa wa upungufu wa chembe hai 
nyekundu za damu (Anaemia), lakini ugonjwa huo hautomfanya 
asiendelee na mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya.

Timu ya madaktari wa mabingwa wa La Liga wamesema kwamba
 waligundua mpangilio usiofaa wa damu ambao unaathiri uzalishaji
 wa chembe hai nyekundu za damu wakati mshambuliaji huyo 
alipofanyiwa vipimo vya damu.

Neymar, ambaye alijiunga na Barcelona kwa ada ya uhamisho 
inayozidi £50million, ameanza matibabu maalum. 
Barcelona imeaambia Associated Press kwamba kutokana na 
upasuaji aliofanyiwa wiki kadhaa zilizopita wa tonsils 
umesababisha aanze kuugua Anaemia lakini tayari ameanza 
matibabu na jambo hilo halitomzuia kuendelea na mazoezi na 
wachezaji wenzake.
 

No comments:

Post a Comment