aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Thursday, August 15, 2013

MTANDAO WA MAJANGIRI WAITISHA SERIKALI....

 
SERIKALI imesema mtandao wa majangili wanaoua tembo
 
 mkubwa wenye watu walio na uwezo kifedha ambapo wapo ndani
 
 na nje ya nchi .Siri hiyo ilifichuliwa Dar es Salaam jana na Waziri 
 
wa Mali Asili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, wakati 
 
akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukutana na
 
 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii
.Alisema tayari Serikali ina majina ya mtandao unaojihusisha na biashara ya ujangili wa meno ya tembo na baadhi yao wapo pia wafanyabiashara wakubwa waliopo ndani na nje ya nchi."Tayari majina tunayo ya mtandao wa watu wanaojishughulisha na ujangili wa meno ya tembo huu ni mkubwa ambao una pesa nyingi, hauna tofauti na ule wa dawa za kulevya,"alisema 
Alisema sio kwamba wameshindwa kufanya kazi bali wanaendelea
 
 kupata taarifa na wameandaa operesheni hai itakayosaka wale 
 
wote ambao wanahusika na ujangili huo.Aliongeza kuwa
 
 wanaendelea kufuatilia nchi inayonunua meno hayo ambapo
 
 nchi zilizopo Bara la Asia ni miongoni mwa zinazo husikana 
 
biashara hiyo.Ali sema siorahisi ku shinda vita hiyo kwa 
 
kutumia vyombo vya habari.
 
"Mnajua hii ni vita kubwa na ni waambie kuwa vita hii huwezi 
 
kushinda kwa kutumia vyombo vya habari, hivyo Watanzania 
 
kuwe ni na amani na tunajitahidi kuhakikisha tunamaliza tatizo
 
 hili,"alisema.Katika hatua nyingine,alisema
 
 mfumo wademokrasia uliopo unachangia kurudisha nyuma
 
 jitihada mbalimbali zinazofanywa, kwani watu wakikamatwa na 
 
kupelekwa mahakamani kesho yake wanaonekana mtaani.
  
Alisema wanaobainika kufanya biashara hiyo ya ujangili hata
 
 Polisi wamo na wengine wameshafukuzwa kazi na wengine
 
 kusimamishwa, hivyo hizo zote ni jitihada za Wizara 
 
yake.Naye Mwenyekiti wa kamati hiyo John Lembei alisema 
 
kuwa kamati yake imeiomba Serikali kuondoa kodi ya asilimia
 
 tatu ambayo ilipitishwa na bunge kwa ajili ya mfuko wa
 
 maendeleo ya utalii na asilimia kumi ambayo yalikuwa 
 
yanawasilishwa Serikalini kwani inachangia kuondoa huduma za 
 
jamii zilizokuwa zikitolewa kwenye jamii inayozunguka hifadhi
 
 hizo.
Alisema kamati imeomba serikali kama kweli wanataka kuendeleza sekta ya utalii basi kodi hiyo ifutwe vinginevyo hifadhi hazitakuwa salama na ujangili utaongezeka kwa kiasi kikubwa."Hifadhi hizi za TANAPA na ngorongoro ilikuwa miradi ya kusaidia jamii inayowazunguka kwa kuwajengea shule, hospitali, maji, pamoja na huduma zinginezo hivyo kutokana na bunge kupitisha kodi hiyo wameondoa huduma hizo,"alisema Lembei.

No comments:

Post a Comment