aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Saturday, August 3, 2013

DUDE AVUNJA UCHUMBA WA MSANII...!!


STAA wa sinema za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ amesababisha msanii chipukizi, Mboni Mhando aachwe na mchumba’ke aliyetajwa kwa jina moja la JB kwa tuhuma ya usaliti.
Chanzo makini ambacho kiliomba hifadhi ya jina, kimepenyeza habari kuwa tangu JB alipoona habari imetoka kwenye gazeti hili wiki iliyopita kuwa mchumba’ke huyo amenaswa na Dude katika pozi za kimahaba, aliamua kummwaga mazima.
“Walimwagana tangu siku ileile gazeti lilipotoka. JB alikuwa akihisi kusalitiwa siku nyingi hivyo ile stori ikawa tiketi ya kuachana,” kilisema chanzo.
Alipotafutwa JB kuhusiana na ishu hiyo, alikiri kumuacha na kudai hawezi kurudiana naye tena.
“Kifupi sina mpango naye, aendelee tu na huyo Dude wake,” alisema

No comments:

Post a Comment