aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, August 16, 2013

BREAKING NEWS: MRISHO NGASSA AIDHINISHWA KUICHEZEA YANGA - KWA SHARTI LA KUILIPA SIMBA MILLIONI 45

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira 
wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu
 za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea
 timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.

Hata hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex 
Mgongolwa imebaini kuwa Ngasa alisaini mkataba mwingine
 Simba (katika kipindi ambacho alikuwa na mkataba na Azam)
 ambapo anatakiwa kurejesha fedha alizopokea (sh. milioni 30) 
pamoja na fidia ya asilimia 50 (sh. milioni 15) ya fedha hizo 
kwa Simba.

Kamati pia imemfungia mechi sita za mashindano 
(kuanzia mechi ya Ngao ya Jamii), na anatakiwa 
awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha
 kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza
 hadi atakapolipa fedha hizo.

Vilevile Kamati imepitia pingamizi zote zilizowasilishwa
 kuhusu usajili wa wachezaji, kukatiza mikataba ya wachezaji 
na kuzitaka klabu husika ziwe zimetatua masuala hayo hadi
 Alhamisi (Agosti 22 mwaka huu).

Kwa upande wa wachezaji wa kigeni, Kamati imeagiza 
wasiruhusiwe kucheza hadi watakapopata Hati za Uhamisho 
wa Kimataifa (ITC) pamoja na vibali vya kufanya kazi nchini 
(work permits).

Kamati hiyo itakutana tena Ijumaa (Agosti 23 mwaka huu) ili
 kupata ripoti za pingamizi ilizoagiza ziwe zimefanyiwa kazi 

hadi Agosti 22 mwaka huu na kutoa uamuzi kwa pande ambazo 
hazikuafikiana.

No comments:

Post a Comment