aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, August 16, 2013

al shabaab wapora MSF Somalia

Ripoti kutoka Somalia zinasema kuwa wapiganaji wa kundi 
la wanamgambo wa kiislamu la al Shabab wameanza 
kupora kliniki zinazomilikiwa na shirika la kutoa msaada wa 
kitabibu la Medicins Sans Frontiers, MSF, baada ya shirika 
hilo kutangaza kuwa linajiondoa kutoka nchini humo.
Wenyeji katika eneo la Bay kusini magharibi wamesema 
waliona wanamgambo wakipora madawa, kompyuta pamoja 
na mitambo mingine kutoka katika makao makuu ya shirika 
hilo.
Siku ya jumatano, shirika la MSF lilisema kuwa linasitisha 
shughuli zake zote kufuatia mashambulizi ya mara kwa mara 
dhidi ya wafanyikazi wake.
Tangu shirika hilo lianze kufanya kazi nchini Somalia mwaka 
1991, wafanyikazi wake kumi na sita wameuwawa.
Wengine wawili walitekwanyara mwaka 2011 na kuachiliwa hivi maajuzi.

No comments:

Post a Comment