aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 21, 2013

UVCCM ZANZIBAR WASEMA "MAALIMU MAALIM SEIF NI DIKTETA "

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Zanzibar,  umemtuhumu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) kuwa  ni kiongozi mwenye viashiria vya udikteta. 
Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM, Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka, alitoa kauli hiyo juzi katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Shaka alisema kitendo cha kiongozi huyo kukataa  kuachia  madaraka ya kisiasa na kulipisha kundi la vijana ni udikteta usio na mipaka ndani na nje ya Bara la Afrika.
Alibainisha kuwa inasikitisha kusikia kiongozi huyo akitangaza kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani ilhali alishindwa mara nne katika chaguzi zilizofanyika miaka iliyopita.
Tangu mwaka 1992 hadi leo Maalim Seif ameshikilia vyeo ndani ya CUF, amekuwa Makamu Mweyekiti wa CUF, mgombea urais  wa kudumu, sasa Katibu Mkuu na hataki kuachia ngazi ili kuwapa nafasi vijana, ndiyo maana nasema ni dikteta hatari,” alisema.
Shaka aliongeza kuwa laiti Maalim Seif angelikuwa anaheshimu misingi ya demokrasia na kutambua umri wake asingeendelea kushiriki siasa kama alivyoahidi hivi karibuni kuwa hataacha siasa hadi aishiwe nguvu.
Shaka aliwataka vijana wa CUF  kujiondoa katika chama hicho na kujiunga CCM ili waweze kupata nafasi ya kuonyesha uwezo  wa kushikilia nafasi za uongozi ambao sasa unahodhiwa na Maalim Seif.
Tazameni CCM ilivyo, vijana  tunapewa nafasi ili kuonyesha uwezo na vipaji vyetu kisiasa, mkibaki huko hadi mtazeeka hamtapata nafasi ili kuisaidia nchi yetu kimaendeleo,” alisema.
Aliongeza kuwa CCM inaonyesha kuheshimu misingi ya demokrasia tangu utawala wa TANU na ASP, ambapo kulikuwa na mabadiliko mbalimbali ya viongozi wa  ngazi za kisiasa na kiserikali, tofauti na vyama vingine ikiwamo CUF.
Alitolea mfano kuwa kwa upande wa Jamhuri ya Muungnano aliondoka madarakani Rais Julius Nyerere  akampisha Ali Hassan Mwinyi ambaye alimuachia  kijiti Benjamin Mkapa na sasa taifa linaongozwa na Rais Jakaya Kikwete.
Alisema kwa upande wa Zanzibar,  Rais wa Kwanza ni Abeid Aman Karume, akafuatia Aboud Jumbe Mwinyi aliyempisha Idris Abdul Wakil, baadaye  Dk. Salmin Amour, akafuatia Dk. Amani Karume na sasa nchi  inaongozwa na Dk. Ali Mohamed Shein.
Shaka alilaumu utendaji aliouita ni legelege, usio wa uwajibikaji  na  uadilifu  kwa wizara ambazo ziko  chini ya upinzani na kusema waliopewa dhamana za madaraka hayo wameshindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo.
Aliitaja Wizara ya Afya chini ya Waziri Juma Duni Haji kwamba haiwatendei haki wananchi huku katika Hospitali ya Mnazi Mmoja mambo ya utawala na utoaji wa huduma  yakiendeshwa shaghalabaghala.
“Duni umepewa dhamana na Rais Shein ila hutimizi wajibu wako, hakuna huduma za kuridhisha Mnazi Mmoja, wafanyakazi, wauguzi na waganga wanalalamika, kutana


No comments:

Post a Comment