aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, October 25, 2013

PICHA: AJALI MBAYA MKOANI IRINGA, WATU 38 WAJERUHIWA


Daladala aina ya Toyota Coaster lenye namba za usajili T 960 AQY linalofanya safari zake mjini Iringa mara baada ya kugongana na lori aina ya Isuzu lenye namba za usajili SM 3363 katika Mlima wa Ipogolo eneo la Kisima cha Bibi mkoani Iringa.
 
l_dd9a2.jpg
m_74746.jpg
Taxi ambayo nayo ilihusishwa katika ajali hiyo ikiwa eneo la tukio, huku askari polisi wakilinda usalama wa mali za abiria.
n_7bc78.jpg
Wananchi wa mji wa Iringa wakitazama ajali hiyo katika mlima wa Ipogolo.
 
o_fbf87.jpg
Coaster likiwa nyang'anyang'a baada ya ajali hiyo ambayo imejeruhi watu zaidi ya 38.

ZAIDI ya abiria 38 wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari manne mjini Iringa, baada ya daladala aina ya Toyota Coaster lenye namba za usajili T 960 AQY linalofanya safari zake mjini Iringa kufeli breki na kuyagonga magari matatu.
Ajali hiyo limetokea katika mlima wa Ipogolo, eneo maarufu mjini Iringa kama "Kisima cha bibi" jana baada ya Coaster kuyavaa magari matatu ambayo ni lori aina ya Isuzu la Manispaa ya Iringa, Tax pamoja na Hiace.
Majeruhi 38 katika ajali hiyo wamelazwa kwenye Hospitali ya Rufaa mkoani Iringa.
Akizungumzia hali ya majeruhi wa tukio hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa Iringa, Dk. Deogratius Manyama amesema wamepokea majeruhi 38 na waliolazwa ni 8 huku majeruhi watatu wakiwa na hali mbaya na kuwa majeruhi wengi wameumia zaidi kichwani na kifuani, huku majeruhi 27 wakiruhusiwa kurudi nyumbani kutokana na kutokuwa na majeraha makubwa.

No comments:

Post a Comment