aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, November 8, 2013

MADENTI WAMLILIA MWENZAO ALIYEJINYONGA BAADA YA KUFELI MTIHANI WA KIDATO NNE...!!

Mwanafunzi  aliyejinyonga  baada ya kufeli mtihani wa kidato cha nne...
Khamis Mkundo Kijana aliyejinyonga.

MADENTI wa Shule ya Sekondari Sabasaba na Kituo cha Krelluu mjini hapa wamemlilia mwenzao, Khamis Mkundo aliyejinyonga kwa hofu ya kufeli mtihani wa taifa (Necta) wa kidato cha nne, mwaka huu.

 
\Hii ndo barua ya  Khamis Mkundo aliyoiacha kabla ya kujinyonga.

Denti huyo, mkazi wa Mwangata C mjini hapa aliwaliza wenzake aliokuwa akisoma nao Sabasaba na baadaye kwenye kituo hicho ambapo alikuwa ‘akiristi’ baada ya kufeli mtihani huo zaidi ya mara moja.

Wana usalama wakisoma barua aliyoiacha denti huyo.

Inauma sana, marehemu alikuwa akijitahidi sana kusoma, tuliweka mikakati ya pamoja ili tuweze kufanya vizuri mwaka huu lakini ghafla tukasikia amejiua,” alisema mwanafunzi mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.
Jamaa huyo alijiua Jumapili iliyopita kwa kujinyonga kwa kamba na kuacha barua ndefu iliyosomeka kuwa amefanya hivyo si kwa kupenda, ila alichukizwa na hatua yake ya kufeli mara kwa mara akajiua ili kuepuka aibu hiyo.


No comments:

Post a Comment