Aina fulani ya unyanyasaji iliyojificha ambayo inajulikana kama ‘breast ironing,’ ambapo wasichana wadogo kuanzia miaka 10 wanachomwa maziwa yao na vitu vya moto ili kuyazuia yasikue inasemekana inafanyika UK sasa.
Unyanyasaji huu wakimila za kikameruni uliwekwa ili kuondoa matamanio ya kimapenzi ya wanaume,mimba zisizohitajika na ubakaji kwa kuzuia dalili za kuwa mtoto wa kike anapevuka/anakuwa mtu mzima,gazeti la independent liliripoti.
Kwa wajuzi wanasema kuwa maelfu ya wakameruni wanaoishi UK wanafuata mila hii.
Kuchoma matiti (Breast ironing)inatambulika na UN kama moja ya makosa ya jinai dhidi ya wanawake na kwa makadirio wasichana wadogo milioni 3.8 wameathiriwa na mila hii.
Ukiachia mbali kuwa ina maumivu makali,pia mila hii inahatarisha afya ya wasichana hao na kusababisha magonjwa na titi moja au matiti yote kupotea.
Source:Latestnews
No comments:
Post a Comment