aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, October 14, 2013

MTOTO WA NYERERE AVUNJA UKIMYA NA KUAMUA KUFUNGUKA YAKE YA MOYONI...!!

Mtoto wa kwanza wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aitwaye Madaraka, amesema viongozi wa sasa wameshindwa kufuata nyayo za kiongozi huyo kutokana na sababu ambazo amesema “haziko wazi”.
Katika mahojiano yake na gazeti hili, Madaraka anasema: “Mazingira ya sasa hayaruhusu malengo ya uadilifu kuenziwa kwa sababu nafasi za umma zinakubalika sasa kuwa ni maeneo ya kujinufaisha mimi kwanza, halafu Tanzania Mungu akipenda”.
Yafuatayo ni mahojiano kamili na Madaraka.
Mwananchi: Ni miaka 14 sasa tangu kufariki kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, unaizungumziaje miaka hiyo kimaisha katika familia, bila kuwapo kwa Mwalimu?
Madaraka: Binadamu tumeumbwa na uwezo wa kukabiliana na kuondokewa ndugu na jamaa zetu wa karibu. Majonzi yalikuwa makubwa baada ya kufariki Mwalimu, lakini tunatambua kuwa kuna umuhimu wa kuomboleza na baadaye kuendelea kukabiliana na changamoto za kila siku za maisha. Na yeye angetarajia hivyo.
Mwananchi: Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi wa nchi, ni zipi fikra au mtazamo wako jinsi viongozi wetu wa sasa wanavyomuezi kwa kuwa wafuasi wa nyayo zake?
Madaraka: Hebu tuseme tu bila unafiki kuwa katika masuala mengi ya uongozi, hasa ya uadilifu, suala la kumuenzi Mwalimu Nyerere ni lengo ambalo viongozi wengi wa sasa wanaweza kuwa wanalo, lakini kutokana na sababu ambazo haziko wazi basi hilo lengo siku zote halikamatiki, liko hatua kumi mbele yao. Na kila wakielekea kama kulifikia na kulitimiza basi wanateleza na kuanguka na lengo hilo linawaacha hatua nyingine 20 mbele.
Mazingira ya sasa hayaruhusu malengo ya uadilifu kuenziwa kwa sababu nafasi za umma zinakubalika sasa kuwa ni maeneo ya kujinufaisha mimi kwanza, halafu Tanzania Mungu akipenda.
Mwananchi: Miongoni mwa mambo ambayo Mwalimu Nyerere aliyaenzi na kuyasimamia enzi za uhai wake, ni Muungano. Kwa maoni yako unadhani hili linaenziwa vipi? (rejea mvutano wa sasa wa Serikali mbili, tatu nk, unatokana na mchakato wa Katiba Mpya).
Mwananchi: Nitumie msemo wa kisiasa kuwa sasa hivi suala la kutengua Muungano linazungumzika. Wakati waasisi wenyewe wapo hai wale waliofikiria kutengua Muungano walipata kigugumizi au walishindwa kuwa wazi na fikra zao. Sasa hivi inaelekea kuna baadhi ya makundi ya viongozi pande zote mbili za Muungano hawataki Muungano, lakini wanashindwa kuwa wazi kutetea msimamo wao huo. Ni sauti chache sana utazisikia zikisimama bila kutetereka kutetea kuwepo kwa Muungano.
Ni dhahiri kuwa sauti za kutaka Zanzibar iachane na Muungano zimekuwa na nguvu zaidi kuliko zile ambazo zinatetea Muungano. Naamini kuwa viongozi wanaozungumzia Muungano wa mkataba hawajapata ujasiri wa kisiasa wa kusema kuwa hawataki kabisa Muungano.

Naweza kuwa siko sahihi, lakini naamini kuwa yeyote anayejaribu kutetea umoja mkubwa zaidi kati ya Bara na Visiwani na siyo mfano tu wa umoja anapingana na mtazamo uliojengwa juu ya fikra kuwa maendeleo ya Zanzibar yanakwamishwa na kuwepo ndani ya Muungano.

source: Mwananchi

No comments:

Post a Comment