aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Saturday, October 5, 2013

HUU NDIO WARAKA WA MWANAMKE ALIYEONGOZA MASHAMBULIZI WESTGATE AKIONYESHA WATOTO WAKE ANAOWAANDAA KUWA MAGAIDI KAMA BABA YAO..!!

Maelezo yaliyoandikwa kwa mkono kwenye kurasa 9 na mwanamke anayetafutwa zaidi duniani, Samantha Lewthwaite aka ‘White widow’ yameonesha jinsi alivyonuia kupandikiza mzuka wa kigaidi kwa wanae.
article-2444552-1884102300000578-392_634x427Magaidi wa baadaye? Samantha Lewthwaite aliandika kuwa anawaandaa wanae, (pichani) kuja kuwa magaidi kama baba yao
Karatasi hizo, zilipatikana kwenye nyumba aliyokuwa akiishi nchini Kenya ambapo yeye na wanakarakati wengine wa kiislamu walikuwa wamepanga kushambulia hoteli mbili na kituo kikubwa cha manunuzi,.
TERROR SUSPECT, SAMANTHA LEWTHWAITE BACKGROUND-PICTURE BY MARK RICHARDS
Nyumba ya Kenya ambayo Samantha anadaiwa alikuwa akiishi

TERROR SUSPECT, SAMANTHA LEWTHWAITE BACKGROUND-PICTURE BY MARK RICHARDS
article-2444552-1884976300000578-496_634x180
Polisi pia waligundua risasi za AK-47 na picha za watoto wanne wa mwanamke huyo. Karatasi hizo zimeonesha kuwa anakuza watoto hao wafuate nyayo za baba yao, Germaine Lindsay aliyejitoa mhanga na kuua watu jijini London.
article-2444552-1884975400000578-929_634x814
Watoto wake wadogo, Abdur-Rahman mwenye miaka mitano na Surajah, 3, ni watoto wa gaidi aliyezaliwa London, Habib Saleh Ghani. Lewthwaite anatuhumiwa kupanga mashambulio kwenye maeneo ya Kenya yenye watalii wengi.

article-2444552-1884976300000578-571_306x423
Mwanamke huyo aliyebadilisha dini na kuwa muislamu, anakisiwa pia kuhusika kwenye shambulio la mwezi uliopita kwenye jengo la Westgate jijini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa. Watoto wake aliozaa na Lindsay, Abdullah, 9 na Ruqayyah, 8, wana majina ya kati Shaheed na Shahidah.
Mombasa
Lewthwaite alikuwa na ujauzito Ruqayyah kipindi Lindsay alipojilipua. Inadaiwa kuwa alikuwa amejificha nchini Tanzania au Somalia. Kwenye maelezo hayo, mwanamke huyo anaeleza jinsi alivyobarikiwa kuwa na mwanaume mgambo na jinsi alivyojitolea kuyaacha maisha ya raha kupigana na wasio waislamu.
article-2444552-1884978B00000578-222_634x720
Source: DAILY MAIL

No comments:

Post a Comment