Msanii wa kundi la Necessary Noise la Kenya Nazizi Hirji amethibitisha kutengana na mume wake baada ya ndoa yao kudumu kwa takribani miaka mitano.
Nazizi alithibitisha juu ya taarifa hizo alipofanya mahojiano na Nairobi News na kuongeza kuwa hawezi kutoa taarifa zaidi lakini ni kweli ndoa yao imefikia ukingoni.
“Siwezi kutoa taarifa zaidi kuhusu hilo, lakini ninaweza kukuthibitishia kuwa ndoa imevunjika.”Alisema Nazizi.
“Ilikuwa ni vigumu kuishi Lamu, nilihitaji kurudi Nairobi ambako wanafamilia wangu wote wako”.
Nazizi alimalizia kwa kusema yeye na aliyekuwa mume wake ambaye wamefanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume bado wanazungumza licha ya ndoa yao kuvunjika.
Source: Nairobi Wire, Via BONGO5
No comments:
Post a Comment