Dereva wa boda boda Cheni Abed akiwa chini baada ya pikipiki yake
kugonga na baiskeli kwenye makutano ya barabara za Mafisa,Kichangani.
Dereva wa boda boda Aliyejulikana kwa jina Bw Cheni Abed kufariki dunia
baada ya
kugongana na baiskeli huku dereva wa baiskeli hiyo ambaye pia alimpakia mwanae
wakiwa salama salmini.
Cheni ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Mchuma kata ya Kichangani mkoani
hapo
alipoteza maisha baada ya kugongana na baiskeli hiyo na kuangukia kichwa
kwenye makutano ya barabara za Msamvu,Mafisa,Mwembesongo huku dereva
wa baiskel hiyo ambaye alimpakia mwanae wakisalimika kwenye tukio hilo.
Umati wa watu ukishuhudi tukio hilo la aina yake
Kufuatia mazingira ya tukio hilo familia ya dereva boda boda huyo iliamua
kusafiri hadi wilaya ya mvomero kwenda kwa mganga wa kienyeji kuchunguza
mazingira ya kifo hicho ambapo Sangoma Hamis Masai mkazi wa kijiji cha
Changarawe kata ya Mzumbe Wilaya ya Mvomero mkoani hapo alimueleza baba
wa mzazi wa marehemu huyo Bw Abed Shabani kwamba mama yake mzazi ndiye
alimuua mjukuu wake huyo kwa kumchukua msukule na kwamba Sangoma huyo
alimhakikishia Mzee Shabani kwamba alikuwa na uwezo wa kumrejesha dunia
mwanae huyo aliekuwa nguvu muhimu kwenye familia hiyo.
Kufutia kauli hiyo Mzee Shabani aliludi Morogoro mjini na kusitisha mazishi ya
kijana wake kwa siku nne akisubiri mganga huyo amfufue, kufuatia taarifa hizo
majirani ambao tayari walishaanza kutoa msaada wa kuchimba kaburi na kuchanga
michango ya mtaa walizuiwa kufanya shughuri hizo kwa maelezo kwamba Cheni
angefufuliwa.
Habari za kufufuka kwa boda boda huyo zilizagaa kwa kasi kubwa kama
kile
kimbunga cha sunami na kwamba siku ya nne aliyoahidi mganga huyo
kumfufua boda boda huyo ilipofika umati wa watu kutoka kona zote za mji wa
morogoro walifuka nyumbani kwa mzee Shabani akiwemo waandishi wa habari hizi
kwa lengo la kushuhudia maajabu hayo. Na Dustan Shekidele..
Familia hiyo na wananchi hao walisubiri toka saa mbili asubuhi hadi
saa moja usiku bila kushuhudi boda boda huyo akifufuliwa na kwamba
Sangoma huyo alipoulizwa na familia hiyo alidai kwamba kuna mashariti
yalivunjwa
na familia hiyo hivyo asingeweza tena kumfufua marehemu wao na kwamba
baada
ya kauli hiyo watu walitawanyika na kurudi siku iliyofuta kumzika boda boda
huyo.
Katika mazishi hayo kuliibuka mambo kadhaa ambapo miongoni mwa mambo
hayo ni mashekhe wote wa kata ya kichanga kugoma kwenda kumsalia marehmu
huyo wakiitaka familia hiyo kwenda kumwita mganga huyo wa kiennyeji
wanayemuami aje kumsalia marehemu wao.
Familia hiyo baada ya kuona viongozi hao wa dini wamevuta 'Hend Breck'
wameamu kukodi boda boda na kwenda kumfuata shekh Mageta ambaye ana
undugu na familia hiyo na kwamba kwenye mawaidha yake Shekh Mageta akiipiga
madongo familia hiyo kwa kuabudu mambo ya kishirikina.
"Nimepata habari mashekh wenzangu wa eneo hili wamesusia kuja
kwenye msiba huu kwa mambo yetu ya kijinga ya kuabudu ushirikina kijana
wetu amekufa kwa ajari na ameangukia kichwa damu nyingi zimetoka leo
mnaenda kuangua kwa mganga kuchunguza kifo chake na mnadanganywa
eti mganga huyo naweza kumfufua mtu mbona ameshindwa kumfufua naomba
siku nyingine msiludie jambo hili" alisema Shekhe mageta kwenye mawaidha yake.
Mwenyekiti wa mtaa huo wa chuma Bw Nathanael Chacha ambaye alikiri
kupokea taarifa za familia hiyo kumfufua kijana wao alijaribu kuwaambia
wajumbe wake waliokuwa kwenye zoezi la kuchanga pesa za pole kuacha
zoezi hilo.
Jambo la tatu lililojiri kwenye msiba huo ni kwamba kwenye akaunti ya simu
ya marehemu kulikutwa pesa taslimu shilingi laki sita na kwamba dada za
marehmu walihangaika kuzitoa pesa hizo bila mafanikio baada ya kushindwa
kuitambua namba ya siri ya marehmu huyo licha ya kujari kuweka namba ya
siri ya mwaka wa kuzaliwa wa maremu huyo.
Baba mzaza wa marembu Mzee Abed Shabani alipohojiwa na mtandao huu
alikiri simu ya mwanae huyo kuwa na kiasi hicho cha fedha na kudai kwamba
wanashindwa kuzitoa baada ya kutoitambua namba ya siri, habari ambazo
mtandao huu umezinasa zilidai kwamba mchumba wa boda boda huyo ambaye
amezaa naye mtoto mmoja ndiye pekee anayejua namba za siri za simu ya
mpenzi wake na kwamba kuna habari zinadai kwamba wifi zake kwa sasa
wamemficha jambo hilo naye amedai kwamba kamwe hawezi kuwatajia
namba hizo za siri mpaka atakapohakikishiwa mgao wa fedha hizo kwa yeye na
mtoto wake.
Mwendelezo wa tukio hili kwa picha za mazishi usikose kutemebea mtandao huu
kujua mengi juu ya tukio hili ikiwemo ya bibi huyo wa marehemu aliyetumia uchawi
naye kufariki duni kwa Sangoma huyo
Pikipiki yake ikiwa safi haijaaribika popote kama inavyoonekana
Polisi wakimpakia kwenye gari boda boda huyo kwa lengo la kumpeleka
hospitali ambapo kabla ya kufika hospitali boda boda huyo alifia njiani.
Mungu ni mkubwa dereva wa baiskeli hiyo alimpakia mwanae ambaye
hakuumia popote kwenye ajari hiyo
Gari ya polisi ikielekea hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
kujua mengi juu ya tukio hili ikiwemo ya bibi huyo wa marehemu aliyetumia uchawi
naye kufariki duni kwa Sangoma huyo
Pikipiki yake ikiwa safi haijaaribika popote kama inavyoonekana
Polisi wakimpakia kwenye gari boda boda huyo kwa lengo la kumpeleka
hospitali ambapo kabla ya kufika hospitali boda boda huyo alifia njiani.
Mungu ni mkubwa dereva wa baiskeli hiyo alimpakia mwanae ambaye
hakuumia popote kwenye ajari hiyo
Gari ya polisi ikielekea hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
No comments:
Post a Comment