The main purpose of this Blog is to share my knowledge with the world..You Are Warmly Welcomed
Contacts:husseinngenje@yahoo.com
+79264327067
Ads 468x60px
Monday, August 12, 2013
TAMKO LA UMOJA WA WANAZUONI WA KIISLAMU TANZANIA KUHUSU TUKIO LA SHEIKH PONDA
Sheikh Suleiman Amran Kilemile
TAMKO LA UMOJA WA WANAZUONI WA KIISLAMU TANZANIA KUHUSU TUKIO LA SHEIKH PONDA
Sisi, Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania (Hay – atul Ulamaa), tumepokea kwa masikitiko makubwa habari za kushambuliwa na kujeruhiwa kwa silaha za moto, Sheikh Ponda Isa Ponda, huko Morogoro, Jumamosi Agosti 10, 2013.
Hay-atul Ulamaa, imesitushwa na tukio hili linalo uma na linaloumiza na kuleta mshtuko na fazaa katika jamii kama ilivyoshtushwa na matukio mengine kama hili hapa nchini. Hili ni tukio ambalo linaashiria kuwa walio litenda hawaitakii mema na amani nchi yetu.
Tunalaani vikali kitendo hicho na tunaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchukua hatua kali na za haraka dhidi ya wale wote walio husika katika tukio hili lenye kuumiza nyoyo za wengi.
Aidha tunawasihi Waislamu na jamii kwa ujumla kuwa watulivu, wenye subira na wenye kunyenyekea kwa Mola wao katika jambo hili zito, wakati tunasubiri vyombo vya dola vichukue hatua zinazo stahiki dhidi ya wahusika wa tukio hili.
Tunamuombea Sheikh Ponda Isa Ponda Allah Amponye haraka na Am,pe baraka katika umri wake. Amin
No comments:
Post a Comment