aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, August 12, 2013

TAMKO LA UMOJA WA WANAZUONI WA KIISLAMU TANZANIA KUHUSU TUKIO LA SHEIKH PONDA

               Sheikh Suleiman Amran Kilemile
TAMKO LA UMOJA WA WANAZUONI WA KIISLAMU TANZANIA KUHUSU TUKIO LA SHEIKH PONDA

Sisi, Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania (Hay – atul Ulamaa), tumepokea kwa masikitiko makubwa habari za kushambuliwa na kujeruhiwa kwa silaha za moto, Sheikh Ponda Isa Ponda, huko Morogoro, Jumamosi Agosti 10, 2013.

Hay-atul Ulamaa, imesitushwa na tukio hili linalo uma na linaloumiza na kuleta mshtuko na fazaa katika jamii kama ilivyoshtushwa na matukio mengine kama hili hapa nchini. Hili ni tukio ambalo linaashiria kuwa walio litenda hawaitakii mema na amani nchi yetu.

Tunalaani vikali kitendo hicho na tunaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchukua hatua kali na za haraka dhidi ya wale wote walio husika katika tukio hili lenye kuumiza nyoyo za wengi.

Aidha tunawasihi Waislamu na jamii kwa ujumla kuwa watulivu, wenye subira na wenye kunyenyekea kwa Mola wao katika jambo hili zito, wakati tunasubiri vyombo vya dola vichukue hatua zinazo stahiki dhidi ya wahusika wa tukio hili.

Tunamuombea Sheikh Ponda Isa Ponda Allah Amponye haraka na Am,pe baraka katika umri wake. Amin

Sheikh Suleiman Amran Kilemile

Mwenyekiti

Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania.

11/August/2013


No comments:

Post a Comment