aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, August 12, 2013

SHEIKH KYELA ASIMULIA ALIVYOPIGWA NA NONDO MBEYA....


Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya, Nuhu Mwafilangu ameelezea jinsi alivyopigwa nondo alipokuwa akiendesha ibada na kudai kuwa zilikuwa njama za muda mrefu za kundi la Waislamu wanaharakati wanaoipinga Bakwata na aliyempiga alikuwa mwanafunzi wa kidato cha tatu. 

Katika Ibada ya Sikukuu ya Idd, saa 2.15 asubuhi iliingia dosari baada ya kuzuka vurugu kubwa katikati ya ibada hiyo kutokana na muumini mmoja kuinuka ghafla kwenye msikiti mkuu wa Wilaya ya Kyela na kumshambulia Sheikh huyo na watu wengine watatu kujeruhiwa.
Akizungumzia tukio hilo Sheikh Mwafilango mwenye umri wa miaka (76) alisema kuwa vurugu hizo zilitokea katikati ya ibada alipokuwa akiongoza swala na baada ya kumaliza takbira saba.
“Baada ya kuanza kusujudu kwenye ardhi ndipo ghafla nikaanza kupigwa na fimbo mgongoni na ndipo nilipotoa kauli ya kuwaeleza waumini wenzangu kuwa nimevamiwa na nilipopata nafasi ya kuinuka nikapigwa na kitu kama nondo eneo la goti kwenye mguu wa kushoto na mkononi,” alisema.
Alisema kuwa hali ilikuwa ni mbaya katika msikiti huo kwani vurugu zilikuwa kubwa.
“Kumbe yule kijana aliyenipiga mimi hakuwa peke yake bali alikuwa na kundi la watu wengi ambao walikuwa wameshika silaha mbalimbali ikiwa ni pamoja na mkasi, kisu na nondo,” alisema.
Aidha sheikh huyo alisema mbali ya tukio hilo pia Agosti 2, mwaka huu alivamiwa katikati ya ibada ya Ijumaa na mmoja wa watu waliohusika katika tukio hilo na kumnyang’anya kipaza sauti na kumtaka aache kuongoza ibada hiyo.
“Aliyenivamia siku ya ibada ya Ijumaa alikuwapo kwenye tukio hilo la juzi na siku hiyo alichokifanya alitaka mimi niondoke na akamwita kijana mdogo kuwa ndiye aendelee kuongoza ibada hiyo kitu ambacho waumini waliokuwapo walizuia na kuniruhusu kuendelea kuongoza ibada,” alisema.
Alisema baada ya kuvamiwa alitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Kyela na baadaye kwa mkuu wa polisi wa wilaya ambapo alitoa taarifa ya maandishi ya kwamba alivamiwa alipokuwa akiswalisha.

No comments:

Post a Comment