aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Saturday, August 10, 2013

SERIKALI YA RWANDA IMEAPA KUTOWAFUKUZA WATANZANIA...

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Rwanda amesema kamwe hawatawafukuza Watanzania wanaoingia na kutoka nchini Rwanda kwa shughuli mbalimbali kwani tupo ndani ya shirikisho la Afrika Mashariki na hata kihistoria Rwanda haijawahi kuwa na tatizo na Tanzania.

Akizungumzia sakata la wahamiaji haramu wa Kinyarwanda kufukuzwa na serikali ya Tanzania amesema, kila nchi inayo mamlaka ya kufanya vile inafaa lakini ingekuwa vizuri Tanzania ingewasiliana na Rwanda ili kujua wataondokaje na kupokelewa vipi.

Amesisitiza, "Kwa kuwa wenzetu wameamua kufanya hivyo, tupo tayari kuwapokea wananchi wetu" Lakini pia, Waziri huyo amesema waasi wa FDRL ni kikundi cha wauaji wanaojipanga kuangamiza watu fulani nchini Rwanda hivyo wanatakiwa kupingwa kwa nguvu zote badala ya kuwatambua na kuzungumza nao kama kundi halali na lenye nia njema.

Naye Mtanzania Mohammed, amependekeza Rais Kagame na Kikwete wakutane na kufikia suluhu.Pia baadhi ya Wanyarwanda wamelalamikia kutokutendewa haki kwa kutenganishwa na wake,waume, n.k

No comments:

Post a Comment