Huku tetesi mpya zikizuka kila siku juu ya
hatma ya mshambuliaji Wayne Rooney,
kocha wa Manchester United David Moyes
amesema jana Jumanne kwamba hahitaji
kumshawishi mshambuliaji aendelee kubaki
Old Trafford.
Alipoulizwa kuhusu namna Wayne Rooney
alivyolipokea suala la United kukataa ofa
mpya ya Chelsea ya £30m kwa ajili kumsajili,
Moyes alisema, "Sijui, sijamuuliza kuhusu
suala hilo."
Pia wakati akijibu swali la kama atamshawishi
nyota huyo wa England aendelee kubaki kuitumikia
klabu hiyo inayojinadaa kutetea ubingwa wake wa
EPL, Moyes alisema: "Huhitaji kumshawishi mtu
yoyote kuichezea Manchester United."
Moyes alikuwa akiongea na waandishi wa habari
baada ya mchezo wa kirafiki ulioisha kwa sare ya 1-1
dhidi ya AIK jijii Stockholm.
No comments:
Post a Comment